Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nakupongeza kwa kunipa nafasi hii ya kuzungumza. Kamati yangu ni ya Miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Spika na Mheshimiwa Naibu Spika, wanafanya kazi nzuri sana katika Bunge hili na Mheshimiwa Spika yeye ni mlezi wangu na amekuja mpaka Jimboni kwangu amekagua miradi mbalimbali. Kwa hiyo, namshukuru sana, anafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwa Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Mundombinu, wanasimamia kazi kubwa ya Sekta ya Bandari, Uwanja wa Ndege, barabara n.k kwa hivyo nimetazama na nimeona Waziri na Naibu wake wanastahili kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze kitu cha maana kabisa. Mheshimiwa Rais, Dkt. John Joseph Magufuli amesimamia Tanzania na kufanya kazi nzuri kabisa katika awamu yake, Mungu amuweka na uchaguzi huu yeye atarudi. Mimi namuombea kwa Mwenyezi arudi yeye pamoja na mimi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mwenyekiti wangu wa CCM Taifa, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Magufuli hapa Bungeni Bhagwanji Maganlal Mesuria, Baniani peke yake arudi tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naangalia na nakupongeza kwa dhati kabisa Mheshimiwa Rais wangu wa Zanzibar Ally Mohamed Shein, ametekeleza wajibu wake katika awamu yake mpaka leo. Wananchi wa Zanzibar wameridhika, barabara, maji, umeme, shule pamoja na hospitali n.k aliyoyafanya sana na amekuwa kifua mbele. Mungu amuweke Mheshimiwa Ally Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar, amefanya kazi nzuri sana na atazidi kufanya na mimi niko pamoja na yeye na yeye namuomba jina langu anirudishe tena. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, Kamati yangu ya Miundombinu, Mwenyekiti pamoja na sisi Wajumbe tunasimamia Sekta ya Miundombinu kwa hivyo Sekta hii inakuwa ina matatizo mengi, Sekta hii tumepongezwa na Sekta hii ya miundombinu tumesimamia barabara, uwanja wa ndege, standard gauge na tumesimamia bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi katika Kamati yetu zikija taarifa kama hizi basi sisi tunakaa na Waziri, Katibu Mkuu wa miundombinu pamoja na wananchi na tunashirikiana kufanikisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia Bandari, Bandari ya Dar es Salaam inafanya kazi nzuri sana lakini pana kasoro moja tu inahitajika irekebishwe, ishikwe mkono kwa sababu hizi container zinatoka nchi za nje na meli inakaa sana na container hazitoki sana katika bandari kwenda nchi zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo hata wafanyabiashara wanalalamika kwa sababu wanafanya kazi sana TRA, bandari na wale watu wa Shirika la Bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naiomba Serikali, Bandari ya Dar es Salaam isimamiwe na kwamba likija kontena, basi ianze kutoka nje haraka sana. Kwa sababu wafanyabiashara wengine wameamua kutoa mizigo yao kupeleka Mombasa kwenda nchi ya Burundi, Zambia na sehemu nyingine nasi tutakosa mapato. Kwa hiyo, naiomba Serikali isimamie bandari yetu ili kontena zote zipate kutoka kwa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile namwomba Mheshimiwa Rais wetu kuhusu Bandari ya Zanzibar ambayo ina kontena nyingi pamoja na mambo mengine, ni bandari ndogo kabisa. Tunataka tushiriki Muungano wetu kupitia Bandari yetu ya Zanzibar 2020 na kuendelea mbele. Ipanuliwe na tusaidiane kwa sababu sisi ni ndugu moja na tunataka kuboresha Zanzibar na Tanzania. Kwa sasa Bandari ya Zanzibar kontena zinakuja nyingi sana na hakuna pa kuweka. Kwa hiyo, naomba Serikali ya Tanzania tufanye kazi pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia uwanja wa ndege. Terminal III imekamilika, nashukuru sana. Bunge lililopita niliwaambia nitasafiri, kwa hiyo kweli nampongeza Mheshimiwa Rais, nilikuwa naenda India na nchi nyingine. Nilikwenda India nikafuatana na mama mtoto wangu pamoja na familia, nimeshuhudia ndege ile inafanya kazi, inajaa sana. Ndege hiyo wakati wa kurudi vile vile inajaa kwa sababu moja; ndege hii Serikali imeamua kwenda direct. Kwa hiyo, wananchi, watalii wa India na nchi mbalimbali wamekubali kupanda ndege yetu ya Tanzania kuja hapa. Hii itatusaidia na kutuongezea kipato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba jambo moja lingine kuhusu uwanja wetu wa ndege wa Zanzibar. Kwa kuwa sisi ni Muungano, lazima tuboreshe kwa sababu wanakuja watalii wengi na tunapata mapato mengi. Sasa kwa sababu ni Muungano, Zanzibar na Dar es Salaam, Tanzania basi tutaongezea; na tulikwama uwanja wetu wa ndege Terminal II, basi tumalize haraka na tuongeze ndege nyingi kutoka Zanzibar kuja Dar es Salaam zinaunganisha kwenda India na sehemu nyingine. Naomba Serikali isaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, mitandao ya simu pamoja na minara yetu katika mipaka inakuwa na matatizo, wananchi wanakosa mawasiliano. Naiomba Serikali na Mheshimiwa Waziri asimamie Tanzania yetu katika sekta mbalimbali na sehemu mbalimbali hususan kwenye mitandao ya simu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zetu tunajitahidi kufanya vizuri na tutazidi kutengeneza. Namshukuru Mheshimiwa Rais, bajeti yetu kwa upande wa miundombinu amesaidia na amesimamia na tumepata pongezi. Kamati ya Miundombinu pamoja na Mheshimiwa Waziri na Kamati yake, vile vile na Katibu Mkuu wanafanya kazi nzuri, nawapongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Makamu wa Rais, wamefanya kazi nzuri sana kwa Tanzania kwa kutembelea kila mahali mpaka Zanzibar. Kwa hivyo, tunampongeza na Mungu amuweke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naunga mkono Kamati hii pamoja na Bunge. Kwa hiyo, naiomba Serikali yangu ya CCM pamoja na Rais wangu, CCM oyee! Nami nataka nirudi tena. CCM oyee! (Makofi)