Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

Hon. Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Kwanza kabisa, napongeza Kamati zote mbili kwa uwasilishaji mzuri na ushauri mzuri uliotolewa. Sisi kwa upande wa Sekta hii ya Madini kuna hoja kama mbili au tatu ambazo zimejitokeza, nazo ningependa kuchangia kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, Kamati zimeelezea namna ya kuimarisha utendaji wa Shirika la STAMICO. Napenda tu kukueleza kwamba Serikali imeendelea kuimarisha utendaji wa STAMICO kwa kuteua Bodi mpya na Menejimenti mpya ili ifanye kazi kwa ufanisi zaidi ya ilivyokuwa inafanya awali. Tumechagua watu wenye weledi na Mheshimiwa Rais alituteulia Mwenyekiti wa Kamati ya STAMICO, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, anafanya kazi vizuri na kwa kweli Bodi inatoa ushauri mzuri na kwa kweli kazi inaenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile limeongelewa suala la ukosefu wa mtaji. napenda kueleza kwamba Serikali pia imeendelea kuliwezesha Shirika la Madini la Taifa kadri fedha zinavyopatikana. Aidha, STAMICO imekuwa inatumia assets zake na hasa leseni ilizonazo kuzibadilisha kuwa sehemu ya mtaji. Kwa hiyo, ukiangalia maeneo mengi ni kwamba leseni ambazo zinamilikiwa na STAMICO, tunapokuwa tunaingia katika joint venture na makampuni mengine katika miradi hiyo, basi zile leseni za STAMICO zimekuwa ndiyo sehemu ya mtaji. Kwa hiyo, badala ya kutegemea mtaji sana kutoka Serikalini, tumeamua kutumia leseni zetu kuwa kama ni mchango wa mtaji katika miradi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile limezungumzwa sana suala la kupunguza gharama za uendeshaji. Tumepunguza muundo wa Shirika kutoka Kurugenzi zilizokuwa tano, sasa hivi tuna kurugenzi tatu. Hivyo, tumepunguza gharama ambapo zilikuwa zinatumika fedha nyingi kulipa au kuendesha zile kurugenzi kutoka Kurugenzi tano kuwa Kurugenzi tatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumepunguza gharama za uzalishaji wa madini hasa katika mradi wa STAMIGOLD. Tulikuwa tunazalisha wakia moja kwa dola za Kimarekani 1,800 ambapo hata katika mauzo katika Soko la Dunia unakuta wakia moja kwa mfano sasa hivi ni dola 1,400 kwa wakia moja. Kwa hiyo, tulikuwa tuna-produce kwa gharama kubwa, tunapokwenda kuuza tunauza kwa gharama ndogo. Tumeona kwamba Shirika lilikuwa linapata hasara na linatengeneza madeni makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tumepunguza gharama za uzalishaji ya wakia moja kutoka dola 1,800 kuwa dola 940. Hata tunapopeleka katika soko tunakuta wakia moja inauzwa labda dola za Kimarekani, sasavi tumepambana hadi kufikia dola 1,500. Kwa hiyo, tunatengeneza faida. Ile difference ya 1,500 na 940, ile difference tunayoipata, ndiyo faida kwa Shirika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile Shirika limeanza kuuza madini yake. Badala ya kupeleka nje, kwa sababu kupeleka nje kuna gharama na ilikuwa inatugharimu kwa trip moja kupeleka dhahabu nje ya nchi, ilikuwa inatugharimu mpaka shilingi milioni 38, sasa hivi tumeshaanzisha masoko ya madini nchini na tumeamua sasa hivi katika mgodi ule wa STAMIGOLD, badala ya kupeleka nje na kwa sababu bei inajulikana, tunauza katika masoko yetu ya ndani. Hii inatuondolea ile ghrama ya kusafirisha madini yao kupeleka nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ni moja ya hatua ambazo tumechukua na tumeweza kupunguza gharama za uendeshaji. Hatua hizo zimesababisha shirika letu, kama mlivyosikia hapo majuzi, tumeweza kutengeneza faida na tumeweza hadi kutoa gawio kwa mchango wa Serikali, tumetoa kiasi cha shilingi bilioni moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, ahsante sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)