Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

Hon. William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa pongezi kwako kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hizi za leo na katika kuchangia kwangu nilitaka nitoe baadhi ya fafanuzi ya mambo yaliyozungumzwa hasa kuhusiana na Shirika la Nyumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza nataka niseme kwamba huko kunakoitwa kudorora kwa miradi ya National Housing hakuna uhusiano wowote na maamuzi ya Serikali kuhamia Dodoma. Kwa sababu uamuzi wa kufanyia Dodoma umefanywa katika Awamu ya Kwanza, sisi Awamu ya Tano tungepozwa tu kwamba tumetekeleza mambo ambayo yameshindwa kutekelezwa kwa zaidi ya miaka 40. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hakukuwa na uhusiano na siamini kwamba Naibu Wangu Waziri alizungumza haya kwamba tunashindwa kutekeleza miradi ya National Housing kwa sababu tume-divert fund kuja Dodoma kwa sababu miradi ya Dodoma ya National Housing ilikuwepo na ilikuwa na fedha zake. Kwa hiyo, nilitaka niseme kwamba uamuzi huu hauna uhusiano na ile miradi lakini najua ni kweli kulikuwa na matatizo katika utekelezaji wa baadhi ya miradi ya Shirika la Nyumba hasa miradi mikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba lilikuwa limejiingiza katika miradi mingi sana ya gharama nafuu ambayo ndio yalikuwa maelekezo ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi lakini pia ilijiingiza kwenye miradi mikubwa sana ya kibiashara. Sasa ndani ya miradi hiyo kulikuwa na matatizo ya usimamizi, uongozi wa bodi lakini na utekelezaji. Kwa hiyo, kabla hatujafikiria kuingiza Shirika la Nyumba kwenda kukopa hizo fedha wanazotaka zikopwe, nimetoa maagizo kwa bodi mpya ambayo tumeiunda hivi karibuni ambayo naipongeza sana imegundua na imeanza kazi kwa kasi sana. Mambo ambayo tumeyafanya ambayo tumeagiza yafanyike ni kama ifuatavyo:-

(i) Tumeagiza kufanya restructuring ya mikopo, ile mikopo yote iliyokuwa imechukuliwa na kujenga hii miradi mbalimbali mnayoona tumeamua tufanye restructuring ya ile mikopo kwanza tuchunguze na tufanye restructuring na huo utaratibu umeshaanza kuzaa matunda tangu tumeagiza mpaka sasa tumeanza na mkopo mkubwa kwa mfano wa Shelta Afrika peke yake tulikuwa tunakopa kwa dola 17% baada ya kukaa tumezungumza sasa tumefikia asilimia 14 kwa shilingi. Kwa hiyo, tunapitia mikopo yote tunafanya restructuring itatupa nafuu zaidi kuliko hata hiyo kupoteza hizo mnazosema shilingi bilioni 20 kwa mwaka;

(ii) Tunapitia mikataba ndani ya mikataba ya ujenzi ile kuna baadhi ya vifungu ambavyo vilikuwa vinaongeza gharama ambavyo havina msingi na contractors tumewa-engage bahati nzuri ule mradi wa Morocco na huo 711 wa Kawe ni contractor mmoja. Tunapitia ile mikataba ili kuondoa mambo ambayo yalikuwa yanaweza kutekelezwa bila kuwepo na gharama hizi na kupunguza gharama na tukipunguza gharama hizi zitatusaidia wote, zitasaidia Serikali kupunguza gharama ya ujenzi lakini itawasaidia hata walaji, ununuzi wa zile unit tunafikiri hata ununuzi wa zile units zile apartment ulikuwa mkubwa kwa sababu ya baadhi ya mikataba iliyoingiwa, kwa hiyo, tunafanya hili la pili.

Pia mjue ndani ya Shirika la Nyumba kuna joint ventures 194 mikataba yake ina mashaka sana kwa hiyo na yenyewe hii tumeikabidhi tunaipitia upya ili kuona hizi joint ventures hazikuingiwa sasa zipo joint ventures muda mrefu lakini baada ya kuchunguza baadhi ya joint ventures tunafikiri tulipigwa nazo zitatusaidia kupunguza gharama za uendeshaji la shirika.

(iii) Tumeamua hivi sasa kuanzisha na kuendeleza kampuni tanzu ya National Housing ya ujenzi. Tunayo daraja la kwanza ya ujenzi kampuni yetu ambayo kwa sasa peke yake kwa kipindi cha mwaka huu mmoja tumeingia na tunajenga miradi mikubwa 35 ikiwepo ni pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Mara, na Hospitali ya Mkoa wa Mtwara tunakwenda vizuri sana. Miradi hii 35 peke yake itatuongezea faida ambayo itawezesha kukamilisha baadhi ya miradi hii;

(iv) Tumeamua kwamba katika maamuzi ya bodi zilizopita na management waliweza kununuanunua mali nyingi ambazo kwa kweli tunafikiri haikuwa msingi tulikopa pesa lakini wakanunua baadhi ya ardhi kwa mfano Arusha kule na sehemu nyingine. Mali kama zile tunafikiri hazikuwa na sababu kununuliwa kwa fedha za mikopo kwa hiyo bodi inaangalia uwezekano. Bodi ya sasa ina wataalam waliobobea inaangalia uwezekano wa kuuza baadhi ya asset ambazo zilinunuliwa bila kufanya utafiti wa kutosha ili fedha hizi zirudi ndani ya shirika ziweze kutekeleza miradi hii, na kazi inaendelea vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini zile kazi za msingi za ujenzi wa nyumba za gharama nafuu hapa makao makuu hazitaathirika na ndio maana nimesema haina uhusiano wa kuhamia hapa kwa sababu ipo program ya ujenzi wa nyumba za gharama nafuu tulishajenga pale 150 na hivi sasa tunamalizia Iyumbu 68 na mwezi ujao tunaanza apartment 100 hapa Dodoma. Kwa hiyo, hii ni miradi tofauti na hii yote inatekelezwa kwa fedha za ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, kwamba shirika lisipimwe kwa sababu ya ile miradi miwili, kazi za shirika zinakwenda vizuri kuliko wakati mwingine wowote. Hivi sasa miradi mingi sana iliyoko mikoani imekamilishwa na mingi ambayo nyumba nyingi ambazo tulikuwa tunatarajia tuuze tumebadilisha utaratibu, sasa tunataka tuuze kwa gharama nafuu zaidi kwa tenant purchase yaani mwananchi akiingia akipanga kodi yake ile tutaihesabu kama sehemu ya mauzo baada ya muda itakuwa mali yake badala ya kumlazimisha mwananchi aende benki kukopa mapesa mengi alipe interest huku alipe kodi, kwa hiyo kodi yake peke yake itamwezesha kununua nyumba. Nyumba nyingi tunafanya tumefanya Kahama, tunafanya sehemu zote ambapo tunajenga hivi sasa, huo ni ubunifu mpya wa bodi mpya na Serikali ya Awamu ya Tano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilitaka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tukishamaliza kazi hii ya restructuring ya mikopo tukikamilisha kupitia hii mikataba mipya ya ujenzi najua tutapata nafuu kubwa sana. Kwanza hata Waziri wa Fedha sijamwambia tunasubiri tupate return ya restructuring hii na upitiaji wa mikopo hii ndio tujue exactly kiasi gani tunataka kukopa kumalizia na wapi tutakopa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaweza tukachukua hela ya Serikali kwa sababu Serikali ina pesa sio lazima twende benki, lakini tunazo Taasisi hivi sasa tuna Taasisi ya TMRC ambayo inawezesha mabenki kukopesha kama push money kwa ajili ya wajenzi wa nyumba za gharama nafuu tunaweza tukakopa hata huko. Kwa hiyo vyanzo vya kukopa vingi lakini lazima tujikite katika ukopaji wenye tija na ukopaji wa gharama nafuu ambao utatuwezesha kushusha gharama ya ujenzi lakini kushusha gharama za wanunuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mmezungumzia habari ya gharama ya ujenzi lakini hamkwenda zaidi kwenye gharama za wanunuzi wa hizi nyumba, hizi nyumba ni ghali sana. Sasa kwa nini ilikuwa ghali tunafikiri ni kwa sababu yah ii mikataba ambayo wajenzi wenyewe wamekubali kukaa na sisi ili kupunguza hizi gharama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mwenyekiti wa Kamati na Waheshimiwa Wabunge bahati mbaya kwenye hizi Kamati za Bunge sisi mawaziri huwa hatuingii lakini haya ndio maelekezo niliyotoa. Nimetoa maelekezo kwa bodi mpya na inafanya kazi nimeridhika kwamba wameanza vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la mwisho pia nimeagiza bodi ifanye re-structuring ya muundo wa Shirika la Nyumba. Muundo wa Shirika la Nyumba vilevile ulikuwa hauna haki sawa ndani ya watumishi, kwa hiyo, hata utendaji wa kazi ulidorora kidogo. Wako watu wachache walikuwa wanapata zaidi kuliko walio wengi. Kwa hiyo, sasa hivi wamepitia nashukuru kwamba juzi wamekaa Baraza la Wafanyakazi Nashukuru kwamba juzi wamekaa Baraza la Wafanyakazi, tunataka tujenge morale mpya ya watumishi wote wa Shirika la Nyumba ili kasi ya uendelezaji wa Shirika la Nyumba tuanze vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kuwahakikishia kwamba Serikali ya Awamu ya Tano inasimamia vizuri kazi ya Shirika la Nyumba. Mapato ya Shirika la Nyumba hayajatetereka na sasa Bodi hii ambayo tumeiunda inasimamia vizuri. Leo tumeanza kuona uwezo wa shirika lenyewe kuendeleza hii miradi kwa fedha za ndani. Wamebana matumizi na wanaendelea kubana matumizi lakini kuangalia upya hii miradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge wa Kawe asiwe na wasiwasi. Tutamaliza ule mradi wa Morocco Square mwaka huu 2020, lakini pia tutamaliza na ule wa seven eleven. Ila tupe nafasi kidogo tuondoe ile hewa. Ni ngumu sana watu kujua, lakini mwenzenu niko ndani kidogo, nakiri kwamba nafikiri kuna hewa kidogo. Kwa sababu kama re-structuring ya mkopo mmoja umeweza kupunguza, kwanza kuondoa uwezekano wa kulipa kwa dola lakini kupunguza interest kwa 4% kutoka seventeen mpaka fourteen, huo mkopo mmoja tu, tunafikiri tunaweza. Kwa hiyo, tupeni nafasi, tuna uwezo na tutatekeleza hii miradi kwa gharama nafuu inayolipika na tutawapunguzia wanunuzi wa hizi nyumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.