Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi. Kwanza namshukuru Mungu. Pia napenda niwapongeze Wenyeviti wote wa Kamati ya Bajeti na Kamati ya Uwekezaji Mitaji ya Umma, kwa mawasilisho mazuri ambayo yanaenda kusaidia utendaji kazi wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba niipongeze Serikali kwa ujumla nikianza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Watendaji wote kwa namna ambavyo juhudi zao zimeleta mabadiliko katika mashirika haya ya Umma ambayo yako chini ya TR. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niipongeze Kamati ya PIC, imekuwa na ushirikiano mkubwa sana, wanakamati wana ari na mori wa kufanya kazi na ushauri wao wametoa mzuri sana, wa kujituma katika kufanya kazi ya Kibunge kama ambavyo tumeagizwa na wananchi. Kwa uchache pia, naomba nimpongeze Athumani Mbuttuka na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri na kuchukua maoni ambayo Wabunge tunayatoa na wanayafanyia kazi. Tumeona mwaka jana 2019 wametoa ripoti nzuri sana ambayo itakuwa ni msaada kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na suala la uwekezaji kiujumla. Uwekezaji tunapata mapato ambayo hayatokani na kodi. Nami pia naungana na Waheshimiwa Wabunge kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuchukua hatua na kuweza kuanzisha Kampuni ya Twiga Mineral Company ambayo ni muunganiko wa Barrick na sisi na tunahisa 16% ambazo haziwezi kupunguzwa and diluted. Kwenye economic benefit ni 50 kwa 50. Hii ni hatua nzuri ambapo tutaongeza mapato yasiyotokana na kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa wito, tumsaidie Mheshimiwa Rais kwenye almasi kama alivyosema na kwenye Tanzanite. Kwa hiyo, nako tuweze kupata faida zaidi na kuongeza mapato ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia kuzungumzia suala la gawio. Ili tuweze kupata gawio zuri na nchi iweze kufaidika na mapato ambayo hayatokani na kodi lazima tufanye vitu viwili; kwanza, tudhibiti matumizi na pili, tuongeze mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bunge lilitunga Sheria ya Fedha Na. 16 ya mwaka 2015 ambapo inatakiwa gharama za uendeshaji zisizidi 60% lakini mashirika mengi yamekuwa yanazidi hii asilimia. Sasa tuombe TR pamoja na Serikali kwa ujumla kuendelea kusimamia ili kuweza kudhibiti mapato na mwisho wa siku itapatikana faida ambayo itakuwa inaongezeka kila mwaka na gawiwo litakuwa zuri kwa Serikali na kuongeza mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa pili wa shilingi ni kuhusiana na mapato kiujumla kwenye kufanya biashara. Tutoe wito kwa mashirika yote kuwa wabunifu kwenye kuongeza aina za biashara ambazo zitaenda kuongeza mapato; na hii itapelekea faida pia kuweza kuongezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala pia la ukusanyaji wa madeni. Kwenye ripoti na tumekuwa tukijadili kwenye Kamati kwmba taasisi nyingi hazikusanyi madeni ipasavyo. Tunajua kuna taratibu za kifedha ambazo deni likikaa muda mrefu inabidi uliripoti kwenye vitabu na matokeo yake linaenda kupunguza ile faida ambayo inaweza kupatikana. Kwa hiyo, tutoe wito kwa Watendaji wote wa Mashirika kuhakikisha kwamba wanakusanya madeni ili kuondoa hasara ambazo zitatokana na kutokukusanya madeni. (Makofi)

Pia kuna suala la kulipa madai mbalimbali na hasa ya kisheria kikodi. Kwa mfano, watu wamekatwa makato ya mifuko ya jamii kama NSSF lakini hayawasilishwi na ile inapelekea kisheria kuwa na penalty. Kwa hiyo, hili linatakiwa pia lizingatiwe kwa mashirika yetu ili kuondokana na hasara zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sera ya gawiwo, tuombe TR ahakikishe kwamba makampuni yote yanakuwa na sera ya gawiwo kwamba kwenye faida baada ya kodi ni kiasi gani kitaenda kwenye uwekezaji na kiasi gani kitaenda kugawiwa kama faida kwa ajili ya wanahisa wote kuweza kupata mgao wao tumeona baadhi ya mashirika hayana sera ya gawio matokeo yake kiasi gani kigawiwe maamuzi yanakuwa hayafanyiki na yanakuwa hayako consistency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo Kamati yetu ilifanikiwa mwaka huu kukutana na kampuni ambazo tunahisa asilimia hamsini au chini ya hapo, kwa lugha nyingine tunaita minority. Hii imetia chachu kubwa sana kwa haya makampuni, tumeweza kutoa ushauri kwa sababu na sisi tuna hisa na wameweza kulisikiliza sana hili Bunge. Kwa hiyo tuombe kama kutakuwa na njia zaidi ya kuboresha na namna gani ya Bunge kuendelea kukutana na hizi kampuni ambazo tuna minority ziweze kuendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna suala la uwekezaji, kuna wakati sasa tunahitajika sisi wenye hisa tuwekeze zaidi kwenye hizi kampuni za minority. Kwa hiyo, mahali ambapo panaonekana kwamba panatija Serikali isisite kufanya vetting ya uhakika na kufanya uwekezaji ambapo mwisho wa siku tutakuwa na faida inayotokana na huo uwekezaji, return on investment. Kwa mfano, tulitembelea Kiwanda cha Sukari cha Kilombero, tumeona kwamba kikiongezeka uzalishaji utaongezeka, zaidi ya tani milioni moja na laki tano zitakuwa zinazalishwa na faida nyingine wakulima wetu wadogo wadogo wataenda pia na wenyewe kuongeza vipato kutokana na ongezeko. Sasa hivi wanatoa tani kama laki sita na sitini, kwa hiyo, uzalishaji ukiongezeka wataenda kutoa tani zaidi ya milioni moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie na kuharakisha mazoezi yote ya ufuatiliaji, mahali ambapo panahitajika kutoa mtaji, basi wahakiki na watoe mtaji kwa wakati maana mwisho wa siku tunakuwa na gawio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni utekelezaji wa maagizo tuliyotoa mwaka jana, mojawapo ili kurahisisha Ofisi ya TR ni kwenda kwenye TEHAMA ambayo itamrahisishia kwenye kufuatilia mashirika na haya makampuni na tulishauri mwaka jana kwamba waingie kwenye mfumo, lakini kwenye ripoti ya TR, bado wako kwenye mazungumzo. Kwa hiyo tungeomba suala hili liharakishwe ili ufuatiliaji wa haya mashirika zaidi na makampuni zaidi ya 260 uwe unakuwa kwenye finger tips, kwa mfano tumeona makampuni mengi yako duniani lakini wanadhibiti dunia nzima kwa kupitia mifumo hii ya TEHAMA. Kwa hiyo, kwa upande huo itasaidia Ofisi ya TR na pia ikama iweze kuongezwa ili tija iweze kuongezeka kwenye hii Ofisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia pia niombe tuzingatie sana hii Sheria ya Public Corporation Acts ya1993 ambayo ina mazingatio muhimu katika kudhibiti matumizi mbalimbali ndani ya Ofisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. (Makofi)