Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia Kamati ya PAC na LAAC. Nianze kwanza kuipongeza Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi ambayo kwa kweli imefanya kazi kubwa sana. Vilevile nizipongeze Kamati ya PAC na LAAC kwa ripoti zao ambazo wameziwasilisha hapa. Tulipokuwa tunachangia zamani tulikuwa tunasema halmashauri zetu zilikuwa kama vichaka vile vya pesa nyingi tulikuwa tunazipeleka kwenye halmashauri, lakini tunaona miradi haikamiliki, lakini sasa hivi Serikali imefanya kazi kubwa sana ya kusimamia mapato katika halmashauri zetu na tunaona sasa miradi mingi sana inakamilika kwa wakati na mambo yanakwenda sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna machache ambayo nataka kuchangia; jambo la kwanza ni kuhusiana na mkopo, ile asilimia kumi, yaani asilimia nne akinamama, asilimia nne ya vijana na asilimia mbili ya watu wenye ulemavu. Kwanza niipongeze sana Serikali nimeona hata katika ripoti Kamati imesema kwamba ni kitu ambacho ilifanya kazi ikahakikisha kwamba inakuwa Sheria. Kwa hiyo hii ni pongezi pia kwa Serikali yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mchango wangu ni kwamba, nikitoa mfano kwenye halmashauri yangu, imefanya vizuri sana. Kwa mfano halmashauri yetu ina vikundi karibu 1200 na utaona kwa mwaka tukichukua 2018/2019, vikundi 98 viliweza kupatiwqa mikopo karibu milioni 400. Sasa ushauri wangu halmshauri nyingi sana hazina uwezo wa kukopesha, yaani hii pesa tulikuwa tuna imani kwamba akinamama, vijana na watu wenye ulemavu iweze kuwasaidia katika miradi ili waweze pia hata kuchangia kodi Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ushauri wangu ni kwamba, kuwepo na vikundi kwa mfano kuna makundi mengine yanafanya kazi nzuri sana, mtaji wao ni mkubwa wanapewa pesa kidogo inakuwa haiwasaidii, lakini kingekuwepo kiwango ambacho vile vikundi vikubwa viki- graduate wasikopeshwe na halmashauri, pengine kungekuwepo na Mfuko wa Vijana au Mfuko wa Rais, wale sasa wafanyabiashara wakubwa wakubwa wakopeshwe huko ili hawa wadogo waweze kukopeshwa na halmashauri ili na wenyewe waweze kupata ile pesa, vikundi vyao viweze kupata na kuendelea kuliko ilivyo sasa hivi ambapo pesa inakuwa haitoshi wanapewa kidogo kidogo kiasi kwamba inakuwa haiwasaidii wale vijana na akinamama.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine ambalo nilikuwa nataka kuchangia ni kuhusu madai ya wastaafu; kwa kweli wastaafu maana yake ni wafanyakazi ambao wameitumikia hii Serikali yetu kwa muda mrefu. Kuna walimu, kuna wauguzi, kuna wafanyakazi wengi ambao wamefanya lakini wanapostaafu wanacheleweshewa sana malipo yao. Wanakuwa na madeni makubwa sana. Mstaafu anastaafu anaanza kufuatilia lile fao mpaka anaweza akafa, anaweza akaugua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikitoa tu mfano kwenye Halmashauri yetu, unakuta Mwaka 2018/2019 na 2019/2020 wastaafu wanadai fedha kama milioni 81 sasa ukija Mwaka 2020/2021 wale ambao wanastaafu wanahitaji malipo ya karibu milioni 45. Sasa Serikali imeweka mpango mzuri sana, wafanyakazi wote wapo kwenye data wanajua kwamba Mwaka kesho watastaafu. Ni kwanini wasingekuwa wanawaandalia kabisa hawa ambao watategemea kustaafu kipindi kingine ili baadaye kusiwepo na usumbufu ambao wanaupata.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeomba kwa kweli Serikali ingefanya kitu kama hicho ili wastaafu wetu wengine wanakuwa wakishastaafu wanataka kwenda kwao lakini naona hizi pesa wanazodai ni kusafirisha mizigo kurudi kwao. Wastaafu wengine walikuwa ndiyo wanataka wakimaliza anagalau sasa waweze kusihi maisha mazuri lakini matokeo yake sasa wanaugua, wanakuwa wanapata mateso makubwa. Naomba Serikali, wanaostaafu mwakani leo hii iwawekee kabisa unapondoka wapewe cheque zao waweze kuondoka bila ya kuwa na madai mengine yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine ambalo nilikuw anataka kuchangia bado ni kuhusiana na madeni ya Madiwani; wenzangu wamezungumzia sana na mimi ni kwamna jamani Madiwani wetu waweze kulipwa yale madeni yao ya posho na stahiki zao nyingine pamoja na Watumishi hii inawapa motisha ya kufanyakazi vizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna madeni pia ya wazabuni; wazabuni wameweza kzilisha Halmashauri zetu, wamefanya zabuni mbalimbali lakini wanakuwa wanadai muda mrefu na tunajua kwamba hawa wazabuni ndiyo wafanya biashara ndiyo tunawategemea tupate kodi zao sasa kama tukiwa-paralysis wakapoteza biashara zao bado tutakuwa hatujawasaidia. Mheshimiwa Rais amekuwa akisema hawa watu ndiyo wa kuwasaidia maana yake ni watu ambao tunatakiwa na wenyewe tunategemea tuwakamue yaani tuwape maziwa na tukamua, tupate kodi nyingi za kutosha. Kwa hiyo, ningeomba hili pia Serikali ingeliweka vizuri ili kusiwepo na madeni makubwa sana ya Wazabuni.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine ni uhaba wa Watumishi katika halmashauri zetu; wahasibu, walkaguzi, wakuu wa idara lakini ni muhimu sasa Halmashauri au Serikali kuna mamlaka mpya kwa mfano; RUWASA, TARURA wanatoa wale watalam kwenye halmashauri zetu wanapelekwa kwenye hizo Taasisi, kwenye mamlaka lakini kwenye halmashauri sasa tunakuwa hatuna wale wataalam. Kwa hiyo, utakuta halmashauri nyingi hazifanyi vizuri hata kwenye miradi, hakuna wale wataalam. Kwa hiyo, ningeomba pengine hili lingewekwa voizuri kwamba wanapotolewa tu wataalam wowote basi mara moja Halmashauri wanaziba yale mapengo ili ziendelee kufanya vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo jingine nizungumzie kuhusu Serikali kupeleka pesa katika miradi ya kimkakati katika Halmashauri zetu; kumekuwa na tatizo kubwa la kuchelewesha hizi pesa za miradi ya kimkakati pamoja na kuwa na nia nzuri sana ya halmashauri kwamba miradi ya kimkakati isaidiwe ili iweze kusaidia mapato katika halmashauri lakini utakuta miradi imekuwa ya muda mrefu sana kwa hiyo sasa inatia tu hasara lakini tulikuwa tunategemea kwamba kama huu mradi ungepewa pesa kwa wakati ule pengine ungefanyika upembuzi yakinifu, kuna miradi mingine inahitajika pesa kidogo sana ingekuwa imeshakamilika. Kwa mfano; tuna mradi wa machinjio pale kwetu ni wamuda mrefu, mashine zimefungwa muda mrefu mpaka zinaweza zikapata kutu laklini kwa mfano mkitoa pesa tu kidogo ule mradi utaleta mapato makubwa kwenye halmashauri kwa hiyo utasaidia mapato na mambo mengi yatakwenda vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuzungumza hayo niendelee kuwapongeza Mawaziri wote waliopo TAMISEMI na wafanyakazi wote na Kamati zote ambazo zimewasilisha report zao hapa lakini na ambayo tumeyatolea ushauri basi yafanyiwekazi ili tuendelee na maboresho lakini nampongeza pia Mheshimiwa Rais kwa akzi kubwa amabyo amekuwa akiifanya katika nchi yetu na Chama cha Mapinduzi kwa utekelezaji wake wa ilani. Ahsante sana. (Makofi)