Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nafasi niweze kuongea kidogo kuhusu hoja ya Kamati yetu ya LAAC ambayo na mimi ni Mjumbe. Kwa sababu nina muda mfupi naomba niende moja kwa moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda niongelee kuhusu asilimia kumi ya wanawake na vijana pamoja na wanawake na watu wenye ulemavu ambayo inapaswa itolewe na halmashauri kutoka na own source yake. Tumegundua na kwa muda mrefu katika ukaguzi wetu tuliona kwamba kuna madeni mengi ambayo halmashauri haiwezi kulipa kutokana na uwezo mdogo wa kuweza kulipwa madeni ya asilimia kumi, tumeishauri Serikali kuhusu kufuta madeni na Serikali imekubali kwa hili imefuta madeni yete ya nyuma lakini mwaka 2018/2019 michango hii inapaswa kuendelea kulipwa. Ukitazama kwamba Serikali imekubali kufuta hayo madeni, sasa napenda kujua Waziri atueleze kama amefuta madeni ya halmashauri kuna pesa ambazo tayari zilikuwa zimekuwa kwenye vikundi, je na zenyewe zimefutwa? Ina maana halmashauri inakwenda kupata hasara kwa kwa sababu hizi ni pesa ni za own source. Kwa hiyo tunapenda kupata majibu kuhusu hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, halmashauri zinapeleka pesa katika Bohari ya Dawa, lakini wakati mwingine wanachewa kuleta dawa na wakati mwingine wanaleta dawa ambazo zinakaribia kuisha muda wake. Kwa hiyo na hilo tumeliona kwamba si kitu sahihi kuhakikisha kwamba MSD inatoa dawa ikizingatia kwamba halmashauri kazi yake ni kutoa huduma kwa wananchi ni pamoja na afya, elimu na mambo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, iko miradi ya kimkakati, kwa mfano iko miradi ya hapa Dodoma ya stendi kuu ya mabasi na soko, lakini kule Morogoro kuna soko kuu, masoko haya yanachukua gharama kubwa, pia tunapenda kujiuliza pamoja na gharama kubwa zilizowekwa katika miradi hii na hasa masoko, je, watu wa chini wataweza kufaidika na masoko haya? Kwa sababu kwa mfano lile soko la Morogoro tumekuta kwamba katika ziara hilo soko halina mkopo hata kidogo ni pesa zimetoka Serikali Kuu pamoja na ule mradi wa kuboresha Miji. Tunachoishauri Serikali ili miradi hii iweze kutumika vizuri, basi halmashauri hizo zisiweke gharama kubwa katika kupangisha, waweke gharama ambazo zitasaidia watu wengi kuweza kuingia ndani ya soko mle na kuweza kufanya kazi na hatimaye halmashauri kupata mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda particularly kuongelea kuhusu Dodoma; ninayo hoja ya msingi na watu wa Dodoma watanisamehe na hasa Mbunge na Madiwani. Dodoma ina mapato mengi sasa hivi, wanapata mapato zaidi ya bilioni 60, wanayo miradi mikubwa ambayo wanatekeleza ni sawa, lakini Jiji la Dodoma limeshindwa kutengeneza barabara za mitaani, huko mitaani kumeoza. Napenda kusema kwamba, je, hizi barabara ni za nani, ni za Halmashauri ya Jiji, au ni za TARURA, na kama ni TARURA ina maana hawana sensa, hawajui idadi ya barabara zao walizonazo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Sheria tuliyopitisha ni kwamba halmashauri ikiwa na pesa inapaswa kuichangia TARURA ili kuhakikisha kwamba inatengeneza barabara za mitaa. Hatukatai kwamba tuna miradi ya Word Bank, inatengeneza lami katika maeneo mbalimbali katika jiji, lakini kule kwenye mitaa hakuko vizuri. Kwa wale wanaokaa mitaani nafikiri mmeshaona kinachoendelea hapa, mimi mpaka nimejiuliza maswali mengi, hivi hawa Madiwani wa hapa huwa wanasema nini ndani ya Baraza lao la Madiwani, sielewi hata wachokisema, kwa sababu kama Jiji linaweza kuwa na pesa za namna hii, inawezekanaje wasitenge pesa za kuweza kutengeneza barabara hata zile za vumbi, kurekebisha kwa sababu Dodoma ni mahali ambapo ardhi mvua inaponyesha hali inakuwa mbaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema neno hili kwa sababu tumekagua juzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma wanayo mapato makubwa na wanajivuna kwa kweli, wamekusanya, wana hela nyingi. Kwa hiyo tunaomba Waziri na yeye anaishi hapa na wengine wote mnaishi hapa. Tunaomba Dodoma watutengenezee barabara za mitaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)