Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kwanza kabisa pamoja na kazi kubwa, kazi nzuri inayofanywa na Waziri pamoja na timu yake yote, lakini napenda kusema kwamba, naona bajeti hii haija-reflect ile safari tunayotaka kwenda, haija-reflect mapinduzi ya elimu ambayo tunataka kwenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezungumzia tunakwenda kwenye uchumi wa kati, uchumi wa kati tukasema tunahitaji mapinduzi ya viwanda, lakini kunahitajika mapinduzi mengi tu, mojawapo ni mapinduzi ya elimu, tuweze kweli kweli kupata transformational change. Sasa kama safari ni hatua, tuone kabisa hatua inayokwenda, kama nakwenda tuseme Kondoa, basi naona nimetokea Dodoma naona nimefika Aneti, nione nimefika Chemba, mwisho wa siku nifike Kelema na hatimaye nifike Kondoa. lakini kwa bajeti hii na malengo yetu ya muda mrefu ambayo tunataka kuyafikia, kwa kweli Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yako, nafikiri kuna kazi kubwa sana ya kufanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri inabidi tuamue sasa kuwekeza kwenye elimu kwa kiwango kikubwa kweli kweli. Huu uwekezaji tulioufanya sasa hivi katika bajeti, naona hautatufikisha pale tunapotaka kwenda, hiyo nilipenda nianze kuzungumzia kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kwenye hoja mahususi katika bajeti nzima ya elimu. Kwanza napenda kuongelea wanafunzi. Suala la mfumo, muundo na kanuni za ufundishaji na kwa maana ya kutoa mitaala naona haimjengi mwanafunzi wa Kitanzania katika kwenda kuingia umahiri katika soko la ushindani kwa maana ya competence. Sisi hatuko wenyewe, dunia siku hizi ni kijiji na inatakiwa wanafunzi wetu wanapotoka huko nje waweze kushindana katika soko duniani, waweze kujiamini, wajenge uelewa badala ya kujenga kukariri na kufaulu mitihani, wajenge uwezo wa kujieleza, matokeo yake wanapofika huko mbele wana uwezo mkubwa wa kupambana na ku-survive, wanasema survival for the fittest. Sasa kama elimu yetu haitujengi kwenda kuwa fit duniani itatukwamisha sana, tutakuta tu tunaendelea ku-import knowledge kutoka kwa wenzetu, lakini wa kwetu sisi hawatoki kwenda nje nao wakafanye vitu vyao huko. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri ni wakati muafaka kabisa Wizara ikae na kujiuliza, hivi tatizo liko wapi? Tujiulize sana na tufanye tafiti za kutosha sana, tunao Wataalam, tujiulize tatizo liko wapi? Kwa nini output, kwa nini products za wanafunzi wetu siyo mahiri? Kwa nini hatuko competent sana on average? Wapo watu wazuri, wanatokea wazuri, lakini on average elimu yetu hairidhishi. Kwa hiyo katika hili, ningesisitiza sana uwekezaji investment ifanywe kubwa sana kwenye RND kuweza kuhakikisha tunainua ubora wa elimu yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, nataka nizungumzie kwa upande wa Walimu. Hapa hasa ndiyo kwenye kasheshe. Ifike mahali sasa ile dhana iliyopo kwamba Ualimu ni kazi ambayo ni dhaifu, mtu huwezi kujivunia, hatuwezi kuikimbilia, tubadilike kabisa. Ifike mahali Ualimu uheshimike, mtu unapoamua kwenda kusomea Ualimu una-proud kwamba mimi ni Mwalimu. Mwalimu awe na uhakika wa ajira, lakini awe na uhakika wanasema maslahi mazuri, very well paid, waweze kuwa motivated vizuri sana, waweze kuwa na incentives kubwa, lakini mazingira pia ya kazi lazima yawe tofauti sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaowachukua hawa kuwa Walimu, siyo ile ya sasa hivi labda tunakwenda mpaka division tofauti tofauti, Walimu wanatakiwa kuwa top scores, top performance ndiyo wawe Walimu na mwisho wa siku na kama maslahi yako mazuri na wanalipwa vizuri, kila mtu atakuwa ana pride kusema akawe Mwalimu na watu wengi watakimbilia kwenda kufundisha. Ualimu uwe ni kazi ya bright students. Tukifanya hivyo kweli tutakuwa tumefanya transformational change, mwisho wa siku Walimu wetu kama ni wazuri, obviously products zao zitakuwa ni nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lingine, napenda kuchangia kwenye suala zima la polytechnic, Vyuo vya Ufundi. Hapo zamani tulikuwa na Vyuo vya Ufundi Dar Tech, chuo ambacho nilisoma mimi, Chuo cha Ardhi kilikuwa kinatoa Wataalam, Mafundi, lakini sasa hivi vile vyuo vyote tumevigeuza vinapanda hadhi vinakuwa Vyuo Vikuu. Sasa kama kila mtu atavaa tai, kila mtu anataka kuwa meneja, kila mtu anataka kuwa na degree, nani atakwenda site kusimamia kazi? Nani ataingia maabara kuhakikisha kazi za kitaalam zinafanywa vizuri?
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kuwa na Vyuo Vikuu vingi, ni sawa tuwe na Vyuo Vikuu vingi, lakini polytechnic ni muhimu sana kuhakikisha kazi za kitaalam zinafanywa. Rai yangu kwa Serikali, hebu tuache hili suala la degree na tai, lakini tuwe na FTC‟s za kutosha. Arusha tech ziimarishwe, ziwe bora zaidi, ziwe equipped, ziwe resourced ili watu wetu wanaotoka kule wakienda kazini, wawe na uwezo hasa wa kusimamia details za kitaalam. Turudishe polytechniques zetu. Kwa hiyo, pamoja na jitihada kubwa ya kuongeza idadi ya Vyuo Vikuu na kutoa degree, hebu na suala la polytechnique tuliangalie sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, la tano na la mwisho, napenda kuongelea kuhusiana na wataalam, watu wanao-qualify, wamekwishasoma degree zao au kama ni FTC, wametoka wameingia kwenye soko la ajira, tutengeneze utaratibu mmoja wa kuwekeza kwa hawa watu ili wakapate exposure programs, wajifunze, waige utaalam, waige experience. Nchi za wenzetu ambazo kwa baadhi ya taaluma zinafanya vizuri. Nitatolea mfano suala la Madaktari, hata Walimu au Wahandisi, lakini nitatolea mfano suala la Madaktari; watu wawe wanatoka tunawapa Mikataba specific wameshamaliza shule, lakini anapelekwa mtu zaidi ya miaka mitano mpaka hata kumi, si tunawekeza kwa ajili ya generation zijazo? Tunawekeza kwa ajili ya kupata transformation ya elimu yetu kwa ujumla wake, watu waje hapa wana uwezo mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi tu tumeshuhudia Tanzania zimefanyika operations za kwanza kubwa za moyo. Watu wanafunua moyo ule ndani wanazibua mirija iliyoziba, lakini waliokuja kufanya ile operation wanatoka India. Kawaida kuna ushirikiano na Australia, Saudi Arabia na Marekani, basi tuwapeleke Madaktari wetu nao wakasome, tuweke mikataba mahususi, watu wakasome, tukishamaliza kuwekeza kwenye elimu hapa, wakimaliza wanakwenda nje, wakirudi they bring back wealth of experience ambayo itatusaidia sana kubadilisha mfumo mzima wa uwezo na knowledge hapa nchini. Kwa hiyo, nasisitiza sana, katika jambo kubwa tunalotakiwa kulifanya kama Serikali ni kuwekeza kwenye elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumerudia na tunaendelea kuimba kwamba tunakwenda kwenye uchumi wa kati, lakini huu uchumi wa kati bila mapinduzi na transformation ya sekta nyingine hizi kama elimu, pia ni mtihani mkubwa tunaweza tusifike. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Elimu kama pioneer katika Serikali kwenye suala zima la elimu, hebu tuangalie maeneo yote haya, kuanzia mitaala, kuufanya Ualimu uwe ni kazi ya kujivunia, shule zetu za polytechnique pamoja na hawa wataalam tuweze…