Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nitoe mchango wangu kwenye Kamati yetu ya PAC ambayo pia ni Mjumbe. Nieleze masikitiko yangu na ya Kamati kwa utendaji usioridhisha wa TRA. Mwenyekiti amewasilisha vizuri sana na mimi nitaeleza pamoja na mambo mengine nitaeleza moja kati ya changamoto ambazo tulielezwa. TRA imekuwa na ufuatiliaji hafifu wa madeni ya kikodi, TRA kutofanyika mapitio ya kina ya miamala ya fedha ya makampuni mbalimbali ya Kimataifa. Na dosari katiika ukusanyaji wa makusanyo ya kodi katika viwanja vya ndege. TRA kutowasilisha kwa wakati mapato inayokusanya kwa niaba ya taasisi nyingine. TRA ina ucheleweshaji usio na tija wa maamuzi ya rufaa ya kikodi, uwepo wa madeni ya muda mrefu yasiyokusanywa. Huo ni mfano wa uozo mwingi ulioko TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ni mfano wa changamoto TRA inayosababishia watu wengine. TRA inaposhindwa kukusanya kodi inatengeneza msururu wa kuleta changamoto kwa wananchi wadogo wadogo ambao wamekuwa wakiteswa na kukamatwa kwa ajili ya kuchangia michango mbalimbali. Utaambiwa michango ya zahanati, michango ya shule, michango ya shule za kata, shule za misingi, watoto wanakaa chini kwa sababu ya watu wazembe ambao wako TRA. Sina uhakika kama ile bahati mbaya au ni makusudi, kwa sababu kama tunaweza tukaajiri watu ambao tunadhani hawana uwezo maana yake hatutaki kukusanya hela ya kutosha na tunazidi kuwaletea changamoto wananchi wetu wa chini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa katika auditing query za CAG kwa mwaka 2017/2018. Ameonesha kuna zaidi ya bilioni 974 kitengo cha kukusanya kodi za ndani yaani domestic revenue department kulikuwa na dosari alihoji CAG wapi kilipo kiwango cha zaidi ya bilioni 679 na TRA waliweza ku-verify kiasi cha bilioni 56 tu lakini kwa walipa kodi wakubwa (large tax payers) CAG alihoji kiwango cha bilioni 607 ikiwa ni pamoja na $ milioni 24 ambayo ni sawa kama na zaidi ya milioni 500. Hizi ukiziweka pamoja unapata kiwango cha shilingi bilioni 974 kama nilivyokwisha eleza awali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hizo hela zote zimekuwa zinahojiwa kwa mwaka 2017/2018. Hizo hela ungeziweka pamoja kwa kiwango cha kujenga zahanati moja kwa shilingi milioni 244 ingejenga zaidi ya zahanati 3,600. Tutakuwa hapa tunasema wanawake wanakufa kwa kujifungua, watoto wanakaa chini, watoto wanapata mimba kwa kutembea umbali mrefu kufuata elimu katika maeneo kadha wa kadha kumbe tuwasababishia sisi changamoto kwa kuweka watu katika taasisi wasioweza kukusanya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati mwingine najiuliza pengine hawa watu sio kwamba wana uwezo hafifu au inafanywa makusdi.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia kuna taarifa. Mheshimiwa Dkt. Ashatu Kijaji!

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumpa Taarifa mzungumzaji kwamba afahamu kwamba katika kipindi ambacho TRA imeimarika kiutendaji, kifanisi ni kipindi hiki na ndiyo maana mwezi wa 12, 2019 tumekusanya zaidi ya trilioni 1.976. Kwa hiyo, naomba alifahamu hilo huku akitambua hayo yalioneshwa kwenye Taarifa ya CAG, 2017/2018 ambayo Serikali tumeshaifanyia kazi kwa kiwango kikubwa na ndiyo maana tumeimarisha ukusanyaji wa mapato. Kwa hiyo, wanapojadili aweze tu kusema sasa wapi tuboreshe zaidi kwa sababu madeni mengi tayari tumeshayakusanya mpaka sasa. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Antropia Theonest unapokea Taarifa hiyo?

MHE ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei lakini nasikitika kwamba anakataa hata Taarifa ya CAG. Moja kati ya changamoto ambayo tutapata kama Serikali ni pamoja na kutotaka kushauriwa au kusikiliza watu wengine wanasema nini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni mjumbe wa Kamatiā€¦

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Anatropia, ngoja tuiweke vizuri kwa sababu Taarifa ambayo Bunge inajadili ni ya 2017/2018 kwa hivyo kwa mujibu wa Kanuni zetu Taarifa uliyokuwa unapewa ni ya kuhusu maboresho yaliyokuja baada ya hiyo Taarifa kutoka. Una uhuru Kikanuni wa kukubali au kukataa lakini sasa sio hoja tena ya Waziri kwamba labda anakataa kupokea unachotoa mapendekezo. Alikuwa anakutaarifu yale ambayo Serikali imeshafanya mpaka sasa. Mheshimiwa Anatropia endelea na mchango wako.

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2017/2018 ni bajeti ya kwanza kuwa na deficit ya 19.7 almost asilimia 20 ya kukadiria ambacho hakitekelezeki kwa almost asilimia 20 kwa maana watu wana expectations au wanajua vyanzo vya mapato lakini hawaendi kukusanya fedha. Ni bajeti ya kwanza kuwa na nakisi kubwa ambayo ilikadiriwa bila kukusanywa. Nadhani Waziri ana nafasi ya kujibu na atasaidia ni namna gani hizo changamoto ataweza kuzitatua katika kipindi kinachokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu ya pili ambayo ililetwa kwenye Kamati ni juu ya kitu kinaitwa immigration. Immigration imeshaongelewa humu ndani zaidi ya mara moja na naiongelea imeletwa kwenye kamati yetu na imesababisha fungu husika kupata hati isiyoridhisha. Mtambo ulionunuliwa kwa ajili ya e-passport haukuwahi kuwa recognized kwamba ulinunuliwa shilingi ngapi, tender ilifanyika wapi? Ulikuwa na gharama gani? Lakini mkataba unahusu nini. Ametumbuliwa juzi Mheshimiwa Kangi Lugola kwa sababu amesaini mkataba ambao haukuletwa Bungeni. Nataka yeyote aniambie hapa, mkataba uliongiwa kwa ajili ya kuleta mtambo wa immigration uliletwa Bungeni? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa Mbunge hapa, uliletwa? Kama tunaamua kufanya haki, tusifanye double standard. Huo mkataba sisi kama Kamati tume-demand uletwe na tuliwafukuza waliokuja kwenye Kamati na jibu walilokuja nalo walisema haya maswali yanahusu usalama, usalama hauwezi kuwa kichaka cha kuingizia hasara Serikali hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu ambacho bado kina-shock, mtambo wenyewe hauko secure, CAG alituambia mtambo hauko secure. Mtu anaweza kuwa nyumbani kwake akawa anachapisha visa, yuko China au kokote anatoa tu Visa sehemu yoyote. Kwa hiyo, sasa ni lazima mjue athari ambayo mnalisababishia Taifa letu kama tunaamua kufichaficha mambo chini ya kapeti. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga Mheshimiwa. Ahsante sana.