Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana ukieleza mambo aliyofanya Rais wetu wa Awamu ya Tano huwezi kuyamaliza. Kwanza nihesabie kuwa tangu nchi hii kuingia vyama vingi sijaona awamu yoyote wapinzani walikuwa ngunguri kuhama vyama vyao kuingia CCM ila Awamu ya Tano Madiwani wamekimbia kwao, Wabunge wamekimbia, hata Wenyeviti wa Serikali za Mitaa. Sifa kubwa anayo Mheshimiwa huyu utendaji wake wa kazi, akizungumza mpaka kule chini vijijini wanapata habari yao. Nidhamu ya hali ya juu imerudi katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi ilikuwa inachezewa, ukitoa ripoti kuhusu mafisadi hawatetemeki, hakuna kutetemeka, leo wanatetemeka vibaya. Hata wizi, wanaoiba wakijulikana hawana nafasi katika nchi hii. Mimi nakaa kwenye mipaka – hawa wanazungumza tu – wamsikie Profesa Lumumba wa Kenya alivyommwagia sifa Dkt. Magufuli; waende Burundi, hawatembei ndugu zangu, wamekaa hapa hawatembei, waende Burundi, waende Rwanda, waende Kenya, DRC Congo, Zambia anavyomwagiwa sifa Rais wetu haijatokea. Hawajapata kuona Rais anayetoa uamuzi mzito kama Rais wetu, miradi mikubwa mikubwa kwa muda mfupi, haijatokea katika Afrika, hakuna cha kumbeza watakaa wanazungumza sisi tunakwenda mbele, hawana jipya kwa sababu Rais kashatangulia mbele hatua 10,000 zaidi yao. (Makofi/ Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, walikuwa Bungeni hapa wenyewe wanalalamika safari za nje, kazibana; wamelalamika hapa mafisadi kawabana. Sasa ndugu yangu hawana jambo jipya, wanayumbayumba washika maji hawa ndugu zangu. Miti yao imeshakauka hata ukimwagia maji mti umekufa umekufa. Nawaomba ndugu zangu upinzani umebaki kama vile jani la mgomba lililokauka.

Mheshimiwa Spika, ndugu zangu, Rais huyu, sikia vyombo vya habari, au labda televisheni na redio za nchi za nje, anavyosifiwa duniani hakuna mfano wake, na bado hasafiri, na bado hasafiri anasifiwa, je angekuwa anasafiri? Ingekuwa balaa. Kafanya mambo mazito katika nchi hii; hospitali mpaka kule Namanyere, mpaka Kirando, mpaka Wampembe kule mwisho wa nchi, hospitali zinang’aa kama mambo ya ajabuajabu.

Mheshimiwa Spika, hakuna sifa zaidi anayopata Mheshimiwa nendeni nchi za nje mkasikilize. Ukifika ametupa heshima ya ajabu, wakisikia unatoka Tanzania kwa Magufuli! umetoka Tanzania nenda popote. Ndugu zangu wamebana safari za nje hawa ndiyo hawajui chochote.

MBUNGE FULANI: Taarifa.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Utatoa taarifa namna gani wewe mimi nazungumza hapa, taarifa ya nini?

SPIKA: Ahsante sana. Mheshimiwa Keissy umeshamaliza.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, Rais amefanya mambo makubwa kwa muda mfupi, haijatokea katika viongozi wa Afrika Mashariki na Kati na duniani. Kajizatiti kwa hela za ndani bila matatizo yoyote…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. ALLY K. MOHAMED: …na wananchi tumuunge mkono. (Makofi/Vigelegele)