Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii nami niunge mkono hatua ambayo imeletwa mbele ya Bunge lako Tukufu ya kumpongeza Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amefanya mambo makubwa sana, hata wale ambao wanapinga wanapinga tu kwa sababu wanajua ukweli. Mheshimiwa Rais ameamua kutengeneza nchi yetu yote bila kuwa na ubaguzi; katengeneza mundombinu ya barabara kila sehemu, tumeshuhudia miradi mingi ya barabara ambayo imejengwa bila kuangalia ukanda, kila sehemu amepeleka miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Spika, amejenga madaraja ambayo yalikuwa hayawezekani kujengwa katika kipindi hicho, jumla ya barabara zipatazo 77 kubwa zimejengwa katika nchi na mikoa mbalimbali. Amejenga na kuboresha viwanja vya ndege; tumeshuhudia Uwanja wa Terminal III ambao ni mkubwa na ni kivutio sasa hivi kwa nchi yetu, lakini ameboresha Viwanja vya Songwe, Viwanja vya Mwanza, Viwanja vya Chato; huu ni uthibitisho mkubwa kwamba sasa hivi nchi yetu inaweza sasa kupokea hata ndege zile kubwa za kimataifa katika eneo letu.

Mheshimiwa Spika, amenunua ndege, zaidi ya trilioni moja zimetumika kununua ndege. Wakati ndege zinanunuliwa watu wengi walibeza na kupinga, lakini cha ajabu ndege ziliponunuliwa wa kwanza kuzipanda hizo ndege ni wale ambao walikuwa wanapinga. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeshuhudia ujenzi na upanuzi wa bandari. Bandari yetu ya Dar es Salaam sasa hivi inapanuliwa na imepokea meli kubwa kwa mara ya kwanza katika nchi yetu hatukuwahi kuona meli kubwa ambazo zinakuja kupakua mzigo. Sambamba na hayo, amepanua Bandari ya kule Mtwara, amepanua anaendelea kujenga Bandari ya kule Tanga; haya ni mapinduzi makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, amejenga Reli ya Standard Gauge ambayo tunaishuhudia, kitu ambacho kilikuwa kama ndoto, leo hii tunaangalia jinsi miundombinu ilivyo na wenzetu wanashuhudia kuona kama kitu cha utalii ambacho kinafanyika katika nchi yetu.

SPIKA: Malizia Mheshimiwa.

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, tunaunga mkono hoja, na ninaamini wewe ni shabiki wa Simba, hata siku moja huwezi ukaungwa mkono na mshabiki wa Yanga; ahsante sana.