Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nilishawahi kusema hapa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sisi wote Watanzania na hili kweli tumelishuhudia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tangu tumepata uhuru hatujawahi kuwa na Naibu Waziri katika Baraza la Mawaziri mwenye ulemavu, lakini ndani ya Serikali hii ya Awamu ya Tano tunaye Mheshimiwa Ikupa ambaye anatuwakilisha vyema. Na hili ni jicho pevu la Rais wetu, Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, lakini sio hilo tu; tunao makatibu wakuu, sio hayo tu, tunaye mpaka Balozi ambaye ni mtu mwenye ulemavu. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, ameandika historia katika nchi hii na tuna kila sababu ya kujivunia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wakati tunachangia kuhusiana na ndege, wakati ndege zinanunuliwa wapo waliopinga, lakini leo hii tunapambana nao kule tukiweka mizigo yetu ambao walikuwa wanapinga. Kwa hiyo, haya yote ni ya kujivunia kutokana na jemedari huyu tuliyenaye, Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

Mheshimiwa Spika, nimalizie tu kwa kusema, 2020 kura yangu chukua, sasa nifiche ya nini Magu uongozi anaujua. Mungu ambariki sana Rais wetu!

WABUNGE FULANI: Asaweeee!

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante.