Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuunga mkono hoja muhimu sana ambayo imeletwa leo kwa Rais wetu mpendwa wa nchi hii. Kwa jina safi la Mheshimiwa Rais anaweza kuitwa a man of all seasons, ni mtu ambaye kwa kweli ametuvusha katika maeneo mbali sana.

Mheshimiwa Spika, mapato ya nchi yetu kwa mwaka 2015 tulikuwa tunakusanya bilioni 800, mpaka jana tunakusanya trilioni 1.9, haijawahi kutokea. Hili si jambo dogo ni jambo kubwa. Tunafanya miradi mikubwa sana ya nchi hii, ukichukua Dar es Salaam tuna mradi wa bilioni 600 infrastructure peke yake Dar es Salaam; tuna Salander Bridge; tuna Tanzanite Bridge; tuna barabara za lami kutoka Mbezi mpaka Kibaha, barabara nane. Sasa haya mambo tatizo mabaharia hawaoni haya mambo. Wakiacha ubaharia watayaona haya mambo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nidhamu ya ukusanyaji pesa, nidhamu ya utumishi, nidhamu ya matumizi, sasa hivi Tanzania inang’aa katika nyanja za kimataifa. Bandari yetu imeongeza mapato, bandari yetu imeongeza meli, sasa hivi ukipita maeneo ya Salender Bridge kuna meli kibao zinangoja kushusha mizigo ya nchini na nje ya nchi, nani kama Magufuli? (Makofi)

WABUNGE WENGINE: Hakunaaaa!

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amepita Jela amekuta watu wameonewa ametoa agizo watu wote walioonewa walitiwa ndani waachiwe, nani kama Magufuli? (Makofi)

WABUNGE WENGINE: Hakunaaa!

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amewafuata mafisadi walioiba pesa amewaambia waliokubali makosa warudishe, warudi kwa wake zao. Nani kama Magufuli? (Makofi)

WABUNGE WENGINE: Hakunaaa!

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Spika, Hospitali zimeboreshwa leo Hospitali za Dar es Salaam ukiingia utafikiri uko Ulaya, Hospitali safi, huduma nzuri na madawa kibao yanapatikana.

Mheshimiwa Spika, tuna ndege, kasema hapa juzi Mheshimiwa Waziri, ndege za mizigo. Tuna ndege ambazo karibuni zitaanza kubeba abiria kutoka Ulaya kuja Tanzania kwa utalii, dogo hilo?

WABUNGE WENGINE: Kubwaaaa!

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Magufuli oyeee. (Makofi)