Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Nami nichukue fursa hii kuunga mkono Azimio la Kumpongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli namna anavyoiendesha nchi hii kuelekea kwenye uchumi wa kati. Ninapofuatilia njia ya Mheshimiwa Rais, napenda niwakumbushe Watanzania wenzangu, tunapokwenda kwenye uchumi wa kati, uchumi jumuishi, tunalenga katika kuwa na maendeleo ya watu ambayo maendeleo ya watu yanapimwa kwa afya na kama walivyosema wenzangu nchi nzima inasheeni, inasheeni vituo vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zamani kwetu sisi tulikuwa tunaona malori yanakwenda vijijini kusomba kahawa, siku hizi tunaona malori ya MSD yanapeleka madawa. Tunapima maendeleo ya watu kwa kuangalia elimu, siku hizi vijana wanakimbizwa kwenda shule na kila anayekwenda shule anapata elimu inayopatikana. Mheshimiwa Rais anajasiria uchumi wa viwanda na uchumi wa viwanda utakapokuwa umefikia katikati tutaweza kukabili vizuri kipato, wako wasioelewa, ujenzi wa uchumi wa viwanda unategemea miundombinu wezeshi na miundombinu saidizi. Miundombinu wenzeshi ndiyo umeme Stiegler’s Gorge, ndiyo miradi mikubwa ya kusambaza umeme, lakini ndiyo hizo ndege, watu wengine hawajaliona. Tunakokwenda tutakuwa na wataalam ambao asubuhi mtaalam atakuwa Katavi, saa sita atakuwa Dar es Salaam, saa tisa atakuwa Bukoba na huyo mtu atatakiwa kuwa Moshi, huwezi kwenda namna hiyo mpaka uwe na ndege kubwa kama bombadier, dreamliner na nyingine ambazo zinakuja.

Mheshimiwa Spika, dunia ya sasa inakwenda kwenye mazao ambayo hatukuyategemea kama alivyosema Mheshimiwa Kamwele, tunakwenda kuleta ndege kubwa za kupeleka mazao, ina maana asubuhi unachuma njungu mawe na maharage ukiwa Bukoba, unakwenda kwenye ndege uwanja wa ndege wa Chato halafu Muhaya aliyeko London anaweza kupata kisamvu na overcado.

Mheshimiwa Spika, tunakwenda kwenye uchumi wa kati, uchumi jumuishi, mambo haya ndivyo yanavyokwenda, huwezi kuijua ngoma mpaka uicheze. Tunaendelea na ujenzi wa viwanda, lakini ujenzi wa viwanda kama nilivyozungumza unategemea miundombinu wezeshi, ICT, wewe mwenyewe na nichukue nafasi hii kukupongeza, sasa hivi makaratasi yale ya mezani hayapo, tulikuwa tunayaacha hotelini, ni mambo ya kubofya tu, hiyo ndiyo miundombinu wezeshi, miundombinu saidizi, ina maana mtu sasa tunapokwenda kesho kwenye TMS, utakapokuwa umevuna kahawa Bukoba au korosho Mtwara, utaweza kumweleza mteja aliyeko China au Vietnam kwamba kahawa yangu ni kiasi hiki na unajua bei, ndiko huko tunakokwenda.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, naunga mkono Azimio hili na namshukuru sana aliyewasilisha Azimio hili, Mheshimiwa Rweikiza ameliwasilisha vizuri sana. (Makofi)