Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, uchangiaji wangu utakuwa reference Ulanga. Mimi naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika nchi yetu ya Tanzania; na sasa mimi nitawapa ushahidi wa Ulanga.

Mheshimiwa Spika, tutaanza kabla mtoto hajazaliwa, yaani kwa maana ya wajawazito jinsi gani Mheshimiwa Rais alivyowajali. Kabla ya uhuru mama zetu wengi walikuwa wanajifungulia kwa wakunga wa jadi, walikuwa wanajifungulia njiani na katika zahanati ambazo zilikuwa hazina vifaa na hata kama zina vifaa, vifaaa vyake ni duni. Vikajengwa vituo zaidi ya 340 vya afya; kwangu nikapata kimoja, kituo hicho cha afya kinaitwa Lupilo. Kabla kituo cha afya hiko hakijaboreshwa kilikuwa kwa mwezi wanajifungua watoto wanaojifungulia katika kituo cha mama wajawazito hapo ilikuwa 25 hadi 30. Baada ya kuboreshwa kujengwa chumba cha upasuaji pamoja na wodi, sasa hivi wanajifungua akina mama 145 hadi 160 kwa mwezi. Hayo ni mafanikio makubwa sana katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa dawa, mtoto anapokuwa, mwanzo bajeti ya dawa ilikuwa kidogo sana na ilikuwa inapatikana kwa mashaka; lakini sasa hivi sio Ulanga nchi nzima bajeti ya dawa imeongezea zaidi ya mara dufu.

Mheshimiwa Spika, mtoto anapokuwa nahitaji kwenda shule, Ulanga sisi tunafuga sana kuku na mifugo midogomidogo pamoja na nguruwe. Ilipokuwa muda wa kufika wa kuwapeleka watoto shule walikuwa wanapita wagambo kuwalazimisha wazazi wawapeleke watoto shule, wazazi wakawa wanalazimika kuuza mifugo yao ikiwemo kuku ili waweze kuwapeleke watoto shule, sasa hivi elimu bure. Idadi ya wanafunzi wanaoenda darasa la kwanza imeongezeka kwa asilimia 56; haya ni mafanikio makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, tumeshuhudia zamani ilikuwa suala la madawati ni la halmashauri na wazazi, tumeanza katika Bunge hili, Bunge peke yake kwa ushawishi wa Rais tumeweza ku-contribute zaidi ya madawati 500 kila Jimbo, haya ni mafanikio makubwa mno.

Mheshimiwa Spika, mtoto anapokuwa anamaliza kidato cha tano na sita anatakiwa kwenda chuo kikuu, tumeshuhudia katika Serikali hii Serikali imetenga mkopo zaidi ya mara mbili kwa ajili ya wanafunzi. Mkopo wa elimu ya juu imefika zaidi ya bilioni 450; haya ni mafanikio makubwa sana. Mwanzo waliokuwa wanasoma shule za private walikuwa hawapati mikopo lakini sasa hivi tumeshuhudia wanaosoma shule za Serikali pamoja na shule za private wote wanapata mikopo haya ni mafanikio makubwa ambayo hayana ubaguzi.

Mheshimiwa Spika, tukija kwenye mawasiliano ndiyo kabisa. Jimbo langu la Ulanga lilikuwa na mawasiliano; kwa sababu wewe ulishafika Ulanga; unaweza ukaongea na simu ukiwa Ulanga pale, Mahenge Mjini ukiwa Minepa pamoja na Lupilo basi yaani jimbo zima lilikuwa na mawasiliano asilimia tano tu. Hivi navyokwambia asilimia 95 ya jimbo lina mawasiliano. Tena kipindi kile kwa bahati mbaya wale wazee ambao walikuwa na wake wawili na watatu ilikuwa ikiingia giza anapotaka kwenda kwa mchepuko anaaga anasema nakwenda kuongea na Mbunge yaani mawasiliano yalikuwa yanapatikana kwenye vichuguu tu ambayo yalikuwa mbali na mji. Kwa hiyo sasa hivi kusambaa kwa mawasiliano kumesababisha hadi kuimarika kwa ndoa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, daraja la mto Kilombero, wewe ni shahidi ilikuwa Ulanga kipindi cha masika huwezi kufika, ilikuwa ni kisiwa. Serikali ya Awamu ya Tano imekamilisha ujenzi wa Daraja la Kilombero. Mimi hata sasa hivi naamua naenda jimboni lakini kipindi hicho muda huu mimi siwezi kwenda jimboni yaani masika Mbunge alikuwa haonekani mpaka masika iishe, hayo ni mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Spika, barabara nchi nzima, kutoka Kidatu mpaka Ifakara ilikuwa ni kipindi cha masika unatumia zaidi ya siku mbili hiyo barabara lakini sasa hivi tunajenga barabara ya lami inapita kwenye Jimbo la Mheshimiwa Lijualikali na Mheshimiwa Profesa Jay hayo ni mafanikio makubwa tu, sio kwa Ulanga kwa nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache na mimi nampongeza Mheshimiwa Rais namkaribisha sana Ulanga, Ulanga wanahitaji wamuone tu, hata asipoongea kitu akifika Ulanga ni ushindi wa kishindo mwaka 2020. ahsante sana. (Makofi)