Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

Hon. Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kuniruhusu nichangie hoja hii ya Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa tukumbuke ilitokea nini mwaka 1977 wakati hapakuwepo Itifaki kama hii kwa ajili ya Kinga ya mali za Jumuiya, Watumishi wa Jumuiya na maslahi mengine ya Kijumuiya zikiwemo fedha nakadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ilikuwa mbaya Jumuiya ilipovunjika nchi wanachama ambao walikuwa na mali nyingi au chache walizuiwa zile ambazo walizokuwa nazo, kwa hiyom nchi nyingine zilipata hasara ikiwemo Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Itifaki hii nianze na Ibara ya 4 ambayo inaongelea kulinda mali za Jumuiya na Ibara ya 5 kulinda fedha za Jumuiya kutonyang’anywa fedha na kutotaifishwa mali lakini pia Ibara ya 8 inaongelea kulinda maslahi ya Watumishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambao jambo hili lilitokea bahati mbaya mwaka ule ilipovunjika 1977 hapakuwa na Itifaki ya hivi Watanzania ambao walikuwa wanafanya kazi kwenye Jumuiya mpaka leo hawajalipwa hela zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hizo ambazo zimezitaja na Ibara hizo ambazo nimetaja katika Itifaki hii naunga mkono Bunge lako kuridhia Itifaki hii ahsante sana.