Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi, nitaenda haraka haraka na niseme tu kwamba sisi kama Tanzania kwa namna moja au nyingine ni Mhimili wa Jumuiya hii ya Afrika Mashariki, kwa hiyo kuridhia Itifaki hii ya Masuala ya Kinga katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kunathibitisha kwamba tuna maslahi mapana lakini tutaendelea kuwa Mhimili wa kuhakikisha kwamba Jumuiya hii inaendelea kuwepo na inaleta matunda mema tofauti na mawazo ya baadhi ya watu wengine wamekuwa na mashaka kwamba pengine siku ikivunjika Vyombo vya Usuluhishi kama vilivyotajwa vitakuwa havipo tutafanya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani tungekuwa na mawazo chanya tukiwa na matarajio kwamba Jumuiya itaenda kutuletea mambo yaliyo mema, lakini kwa haraka niseme kuhusu Ibara ya 6 ambayo inaeleza kwamba nchi pamoja na ile hali ambayo ilikuwa katika Jumuiya iliyopita Itifaki hii ina masuala mazima kwa namna moja au nyingine yanaenda kuzuia nchi kujinufaisha binafsi isipokuwa kwa makubaliano na hakuna nchi itanufaika na mali za Jumuiya kama ilivyotokea mwaka 1977.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaona kabisa ni mambo ambayo yanaendelea kutuweka pamoja, lakini Ibara ya 10 inaonyesha kuwa Afrika tunaweza sasa na tunathibitisha kwamba tunaweza kujiamulia mambo yetu na hii ni heshima kwa wananchi wa Afrika Mashariki kwamba inapotokea mgogoro ni wajibu wetu sisi kutafuta ufumbuzi na hata itakapolazimu kwenda katika Vyombo vya Sheria, kwenda katika Vyombo vya Kimahakama basi tutakwenda kwenye Mahakama ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tofauti na wakati ule ambapo baada ya yale matatizo ilibidi watu Commonwealth waje watusaidie, kwa hiyo hii inaendelea kuthibitisha kama ambavyo sisi katika Tanzania tunaionyesha Dunia chini ya Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwamba kuna mambo tunaweza tukayasimamia na tukayafanikisha na hii Ibara ya 10 inaonyesha kwamba sisi kama wana Afrika Mashariki tumejidhatiti kwamba kama kutatokea matatizo, kama kutatokea migogoro sisi wenyewe tutakaa chini tutasuluhishana, tutawekana sawa na ikilazimu kwenda Mahakamani hatutakwenda The Hague, bali tutabaki katika Mahakama ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, Ibara ya 11 inatoa room ya marekebisho kama kutaonekana kuna jambo tunadhani tuliongeze basi tuweke marekebisho, baada ya kusema hayo naunga mkono. (Makofi)