Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nashukuru nianze kwa kusema kwamba sisi Kamati yetu ya Miundombinu tumechambua sana Itifaki hii na naunga mkono Itifaki hii kwa niaba ya wenzangu kwenye Kamati kwa sababu ni kitu chema sana, chema kabisa, ila nina mambo mawili tu madogo sana na maadamu Waziri wa Mambo ya Nje yuko hapa kwa kweli hoja hii ningeilekeza kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, part two ya Protocol hii inasema kwamba ili Protocol hii ifanye kazi lazima nchi wanachama wote waridhie na mpaka sasa tumepewa taarifa toka Serikali ni nchi tatu tu zimesharidhia Protocol hii kwa maana ya Kenya, Uganda na Rwanda, Burundi bado Southern Sudan bado na kadhi hati yake ni kwamba Protocol hii haitafanya kazi mpaka members stance hawa wawe wamesaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa naomba kwa sababu ni kitu chema sana hiki, kwa kweli ni chema kiuchumi kwa Tanzania nilikuwa naomba nipate maelezo ya Serikali kupitia Secretariat ya Afrika Mashariki, Waziri wa Foreign Affairs kwa kweli mfanye jambo hili haraka kidogo ili wenzetu wa Burundi nao wasaini na wenzetu wa Southern Sudan nao wasaini ili Protocol hii iweze kuwa, iweze kuwa na maana iliyokusudiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili faida yake ya pili nyingine kubwa sana ni Mkongo wa Taifa nadhani Waziri wa Fedha utakubaliana na mimi kabisa kwamba Mkongo wa Taifa sasa ni chanzo kingine kizuri sana cha mapato ya Serikali na Mkongo huu tayari umeunganishwa na Burundi na nchi ya Kenya, sasa kwa sababu ni kitu chema na tunafanya biashara ya ki-digital na wenzetu katika nchi jirani hizi ni vyema kabisa wenzetu wa Wizara hasa Foreign Affairs jambo hili mlipe kipaumbele sisi kwetu ni kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulitizame zaidi Protocol hii kibiashara ili hatimaye Mkongo huu wa Taifa tuweze kuuendesha kibiashara zaidi na hasa masoko yetu yakiwa ni nchi za jirani, la mwisho faida nyingine ya Itifaki hii.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa muda wetu ndiyo huo.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono Itifaki hii. (Makofi)