Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kwa Uamuzi wake wa Kulifanya Bunge Kutekeleza kwa Vitendo Dhana na Bunge Mtandao (e-Parliament)

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kwa Uamuzi wake wa Kulifanya Bunge Kutekeleza kwa Vitendo Dhana na Bunge Mtandao (e-Parliament)

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru Wabunge, wale waliochangia na Wabunge wote kwa ujumla kwa kuona umuhimu wa hoja hii ambayo tumeileta hapa Mezani.

Wabunge wanne wamechangia kwa niaba ya Wabunge wengine wameelezea yale ambayo tumeyazungumza ndani ya Azimio hili la Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuokoa muda, nami naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Spika kwa namna ambavyo ametuwezesha sisi Wabunge kuwa wa kisasa. Cha msingi niombe tu Wabunge waweze kuzitunza ili zisipotee maana zikipotea Bunge tena halitaingia gharama ya kuwanunulia itabidi wanunue wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi na naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.