Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote tena napenda kuchukua fursa hii kwanza kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kupata fursa hii nami kuja kuhitimisha hoja zetu hizi mbili za Maazimio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishukuru sana Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwa michango mizuri na maekelezo mazuri ambayo wanatupatia hasa kwenye Maazimio haya mawili. Naomba niwahakikishie tu kwamba maoni yao, mawazo yao na fikra zao zote tumezichukua na tutakwenda kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia, wameonesha kwa dhati umuhimu mkubwa wa kupambana na emission hizi ili kuhakikisha kwamba na sisi Taifa letu na ulimwengu kwa ujumla unakuwa salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wajumbe wote wamechangia vizuri Maazimio yote mawili; kwanza, Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa Ajili ya Maendeleo Endelevu. Kama tunavyojua kwamba emission hazina mipaka kwa vile ni juhudi za pamoja, zinahitajika kwa nchi zote za SADC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge kwa kuchangia na kutoa msisitizo mkubwa kuhusu Azimio la Kuridhia Marekebisho ya Kigali ya Kupunguza hizi Emissions za HFCs ambazo zina athari kubwa kama alivyosema Mheshimiwa Juma Hamad.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ufupi tu, nakubaliana na Bunge kwamba, kwa pamoja hatunabudi kupitisha maazimio haya kwa sababu zina faidi kubwa ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezieleza hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.