Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Namshukuru Mheshimiwa Waziri Mbarawa, nawashukuru Kamati na Waheshimiwa Wabunge wote ambao wamechangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ijikite hasa katika kujibu hoja za wenzetu wa Kambi Rasmi ya Upinzani. Wamesema yawezekana taasisi ambazo tunazo ni taasisi ambazo hazina viwango, hazina ubora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaeleze tu kwamba, tunaporidhia mkataba kama huu, maana yake Serikali inapata teknolojia, lakini tunapata fedha kwa ajili ya kufanya capacity building. Kwa hiyo, eneo hili tunakuwa tumelimaliza kulingana na utaratibu huo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mwanya wa rushwa, wamesema kuna grand corruption, siyo kweli. Sisi tuna focal point, maana yake hizi nchi wanachama ziko focal point, hakuna bidhaa inaingia kabla Mkurugenzi wa Mazingira hajaridhia. Akisharidhia, maana yake ile bidhaa haina tatizo. Kwa hiyo, hakuna compromise ya kampuni yoyote itakayoingiza bidhaa yake bila sisi kama Serikali na Ofisi ya Makamu wa Rais kukubali kwamba iingie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wamepewa semina. Kam mmemsikiliza Mwenyekiti hapa, ameeleza vizuri kwamba Kamati imeshapata semina na wamekuwa na uelewa mkubwa; na kwa semina hiyo uelewa huo maana yake wametuwakilisha sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili halijaanza leo, nchi imeridhia Mkataba huu wa Vienna tangu mwaka 1993 na kuanzia hapo marekebisho yameendelea. Huu ni mkataba wa sita; tumefanya wa kwanza, wa pili, mpaka wa tano na huu ni wa sita. Kwa hiyo, kama nchi tuna uelewa mkubwa sana kwenye eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge. Nirejee kwa Mheshimiwa Janeth Mbene; ni kweli fungu lipo kama alivyoeleza, linaendelea kwa utaratibu ule ule. Pia namshukuru Mheshimiwa Jitu Soni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zungu ameeleza hoja yake ya msingi sana ambayo nataka kueleza Bunge lako kwamba tunaendelea na utekelezaji kuhakikisha nchi inapata fidia kulingana na uharibifu wa mazingira wa viwanda vya wenzetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Juma Hamad, kwa kweli ametoa elimu ya kutosha sana, Mungu ambariki. Nadhani sasa watu wote wamepata uelewa wa juu ni nini kifanyike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa dakika zako.