Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kwa kunipa nafasi hii niweze kuzungumza kidogo. Na mimi naunga mkono Itifaki hii ya Kigali, lakini napenda kuishauri nchi katika eneo hili kwenye mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, Tanzania tumetangaza kwamba sera yetu ni Uchumi wa Viwanda. Ila moja kati ya vitu ambavyo vinaleta athari ya hizo emission katika ozone layer ni aina ya viwanda ambavyo vinatoa carbonmonoxide kwa kiwango kikubwa. Sasa sijui katika ile blueprint yetu na huo mkakati wa uchumi wa viwanda tumejiandaaje kukabili kiwango kikubwa cha emission ambazo zitakuja kuzalishwa hapa ndani ya nchi, pengine nasi kama Tanzania tukatakiwa tutoe fidia kwa uharibifu wa mazingira ya ozone layer. Sasa hilo natoa angalizo la mwanzo kabisa kwa nchi, tunapokwenda huko tuwe na tahadhari hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, bado ndani ya nchi vile vile hakujawa na mikakati thabiti. Hapo nyuma tuliandaa mpango mkakati unaitwa REDD (Reduce, Emission, Degradation of Deforestation) kwa ajili ya kunusuru emission zote ambazo zinaweza kutokea, iwe kupitia kwenye madawa na kemikali mbalimbali za viwandani, lakini vilevile kwa carbon monoxide ambayo haivunjiki kutokana na miti tuliyonayo kidogo haiwezi kunyonya au kuvuta hewa yote ya carbon monoxide.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine vilevile, ndani ya nchi bado mkakati wa kuwadhibiti watu wenye magari mabovu yanayotoa moshi mwingi njiani na sehemu nyingine haujawekwa na tukaweza kuona kwamba kuna una udhibiti kiasi gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa zaidi ninaloliona, hata viwanda viwanda vyetu vile vya Wazo, hata ile Songwe vile vya saruji vinatoa moshi mkubwa. Ile ni pure carbon monoxide ambayo kuvunjika kwake kunataka kuweko na emission nyinginezo ambazo zinaweza kusaidia kuvunja. Sisi tumeviacha vile viwanda, hatuvishauri katika mazingira haya tuliyokuwanayo. Kwa hiyo, tunachangia na sisi katika uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wito wangu nafikiri Wizara inahusika, ikae na wahusika, tuweke mpango thabiti sasa ambao utaweza kudhibiti huo uharibifu wa mazingira kwa hilo eneo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)