Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Juma Hamad Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ole

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Mimi kidogo mchango wangu utakuwa ni tofauti na wachangiaji waliopita. Kwanza kabisa, naomba kuunga mkono kabisa kabisa, mia kwa mia Itifaki hizi mbili za mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa sababu ni jambo ambalo linatu-affect vizazi vya sasa na vizazi vinavyokuja. Nataka nianze kwa kusema, hii ozone layer hai- belong to any state, wala siyo ya mtu binafsi. Mwenyezi Mungu alipoumba dunia akaweka ozone layer. The question now rise, why should there be no depletion of ozone layer? Ozone layer ina mambo mawili makubwa; moja, ni production of oxgen. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mtu wa chemistry, kwa hiyo, nataka niwalete kwenye chemistry. Nafikiri wale wale waliokuwa hawanifahamu, degree yangu ya kwanza ya Bachelors ni Physics Chemistry, lakini ya pili nime-specialize kwenye Chemistry. Sasa Ozone layer ni producer of oxygen. Oxygen ni hii hewa safi ambayo tunaivuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ozone layer Mwenyezi Mungu kaiweka makusudi siyo kwa bahati mbaya ili iwe ni blanket au insulating sheets ya jua, mionzi inayotokana na jua. Mtakumbuka kwamba jua liko around 93 million miles from earth surface. Kwa hiyo, kama ingekuwa ile mionzi ya jua inatupiga direct, nafikiri hapa kungekuwa hakuna mtu tena, wala kiumbe kisingeweza kuishi katika dunia hii, lakini kwa sababu ya ozone layer ndiyo tunapata protection. Mungu atunusuru, siku za the day of eruption eeh, wanaita siku ya kufufuliwa. Inasema…

MBUNGE FULANI: Rise eruption.

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Yes, rise eruption. Wanasema hili jua litakuwa karibu sana na sisi; nasi tutakaa sana kabla ya kuhukumiwa. Kwa sababu tutakaa sana, jasho lile litakalotutoka litafika mpaka kwenye mabega, wale wenye dhambi kali. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, uwepo wa ozone layer haukufanywa kibahati mbaya na Mwenyezi Mungu. I agree na maazimio haya na hasa lile Itifaki ya Motreal na marekebisho yaliyofanywa nchini Rwanda, nakubaliana nao mia kwa mia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nadhani sisi mwanzoni tulifikiri tatizo la ozone layer kutobokatoboka, kuwa na matundu ni kwa sababu ya kemikali za aina zinazoitwa CFS (Chlorofluorocarbons), lakini baadaye tukagundua kwamba unaweza uka-get rid of chemical inayoitwa chloralfluorocarbons hasa kwenye utengenezaji wa friji, jokofu, air conditions na kadhalika kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge. Tukaja na kemikali mbadala inaitwa hydrochlorolfluorocarbons. Hata hivyo, as we say na kwa mujibu wa protocol hii ya Montreal kuna a lot of chemicals ambazo zinasababisha mmomonyoko wa ozone layer.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo siyo la Tanzania. Nataka nisikubaliane na Kambi ya Upinzani kidogo na wale ambao walikuwa wanafikiri kwamba kuleta friji mbovu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda!

MBUNGE FULANI: Mwongezee!

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe elimu.

MWENYEKITI: Kwa sababu ya field yako hiyo, natumia mamlaka yangu hayo, ongea kidogo dakika tatu zaidi. (Makofi)

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu problem iko katika nchi zilizoendelea. Suala la haya mafriji, majokofu, kutengenezwa kwa kutumia hiyo kemikali mbadala, hydrofluorocarbon siyo tatizo. Tatizo ni kwamba nchi zilizoendelea, zenye viwanda zina a lot of emission ya hizi kemikali ambazo huwa ni distractive. We don’t want to talk of hydrofluorocarbons; na hiyo sasa imeambiwa kwamba nayo ina madhara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri kama sikosei kuna kama kemikali za aina sita ambazo zote ni destructive ya ozone layer. Ukiacha CFS, unakuja hydrofluorocarbon ambayo sasa hivi inatumika katika utengenezaji wa mafriji, lakini kuna hydrofluorobromocarbons, kuna hydrobromochlorocarbons a number of them; kuna hizi chemicals zinazoitwa halons ambazo is nothing but carbontetrachloride. Kuna a lot of chemicals sasa hivi na hizi hatuzalishi sisi, wanazalisha nchi zilizoendelea, zenye viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kusema kwamba friji bovu au kifaa chakavu kitaleta emission hiyo, siyo kweli. Hata ukinunua friji zima jipya, basi kule kuna hydrofluorocarbons. Kwa hiyo, friji inavyofanya kazi, liwe jipya, liwe kongwe lina emission ya hydrofloralcarbons. Tatizo nasema tena ni nchi zilizoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, solution ni nini? Kwanza tuzibane nchi kubwa kwamba ipo side penalt clause katika ile Itifaki lakini is not punitive, wala haitekelezwi. Leo Taifa kama Marekeni, China, Japan, Italy ambazo zina viwanda tukizibana tukawaambia lazima watoe 5% of their budget kusaidia nchi changa kwa suala la kuharibiana mazingira, hilo litakuwa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, au tukazibana tuwe na effort ya pamoja, tufanye reseach ili tupate kamikali mbadala. Hiyo inawezekana. Suala la AIDS, HIV, tuna research ya pamoja na mpaka sasa hivi hatujapata dawa, lakini at least kuna jitihada joint efforts ambazo zinaonekana zitazaa matunda huko baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, mataifa haya makubwa waambiwe wapunguze viwanda ambayo huwa vina-emit hizo hydrofuorocarbons otherwise suala la ozone layer litaendelea. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, again, naomba kuunga mkono azimio hilo. (Makofi)