Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Gimbi Dotto Masaba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nakushukuru, nami naomba kuchangia. Napenda tu niseme kwamba Itifaki hii kimsingi imekuja wakati ambao asilimia 80 za maambukizi ya magonjwa yanatokana na kemikali zinazotokana na madawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo tunazungumza kuridhia Itifaki ya SADC, ni sawa, lakini natoa masikitiko yangu kwamba, pamoja na kwamba tunaridhia Itifaki hii lakini kumekuwa na utaratibu wa kutozingatia umuhimu wa mazingira ya Taifa letu. Ukiangalia bajeti ya mazingira iliyopita ni 0.0. Sasa nilikuwa najiuliza, tunavyozungumza kuridhia Itifaki hii, wakati huo huo Serikali haioni umuhimu wa kuboresha mazingira yetu kupitia bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba tunakwenda kuridhia vitu kama hivi, bado kwenye taarifa ya Makamu wa Rais imezungumzia asilimia 61 ya ukataji wa miti nchi yetu iko hatarini. Kwa hiyo, pamoja na kwamba Serikali imeleta Azimio hili na huku ukizingatia karibu dawa zote zinatumia kemikali, hata ukiangalia kwenye kilimo chetu, dawa tunazotumia kwenye mahindi zote zinatumia kemikali; ukienda kwenye mboga mboga zote zinatumia kemikali; nataka niiulize Serikali, imejipangaje kuhakikisha kwamba inakuja na utaratibu ambao utawezesha kkutupatia dawa ambazo hazina kemikali? Kwa sababu dawa karibu zote zina kemikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzungumzia, kuhusu suala la ozone layer, bado narudi kule kule kwenye bajeti. Kwenye Bajeti Kuu ya fedha za Maendeleo kulikuwa na sifuri, lakini bado fedha za nje tulipata kiasi cha shilingi milioni 500. Sasa najiuliza, Wazungu wanaona umuhimu wa mazingira wa Taifa letu, lakini sisi hata huu mradi wa Ozone Layer hatuoni umuhimu wa kuzuia hili joto ambalo ni hatari kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumza suala la mazingira ni lazima turudi kwenye Sheria Na. 20 ya mwaka 2004 kuhakikisha kwamba inatumika vizuri ipasavyo kuliko ambavyo tunavyozungumza kinagaubaga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)