Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nami nimepata muda wa kuchangia Mpango wa Maendeleo wa 2020/2021. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Ndugu Dotto na wafanyakazi wote wa Wizara ya Fedha. Kusema kweli wanakusanya fedha jinsi inavyotakiwa, lakini nasi Wabunge ndio tunapanga matumizi hapa. Matumizi yanakwenda jinsi inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kidogo, mtaniwia radhi Waheshimiwa Wabunge. Sisi Wabunge lazima tuwe na uchungu na nchi hii kwa sababu, tumeletwa na kura za wananchi ambapo tulikotoka huko wana matatizo ya maji, tunadai barabara mbovu, tunadai sijui TARURA wapewe pesa, sijui nani apewe pesa. Nasi Wabunge vilevile ndugu zangu, tuwe na moyo wa kumsaidia Waziri wa Fedha kuhusu matumizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila siku mimi nakwenda kwenye mazoezi kasoro Jumapili, lakini Waheshimiwa Wabunge hawa; humu ndiyo kuna Kamati za Michezo, Mwenyekiti wao yuko Mheshimiwa Ngeleja na ataniunga mkono mwana-mazoezi mwenzangu ambaye kila siku tuko naye kwenye mazoezi Mheshimiwa Naibu Spika atasema ukweli lillah hapa leo Jumatatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wako wanakuangusha. Hawaendi kwenye mazoezi hata mara moja. Ni wachache sana. Wanakwenda kwenye mazoezi wakisikia kuna safari, kwa sababu wanafuata maslahi. Hawaoni huruma na wananchi waliowaacha kule Majimboni kwetu hawana maji wala chochote. Leo nimeshuhudia, wamesikia kuna safari ya kwenda Uganda, wamejazana kule Jamhuri Stadium kwa makundi, sio akina mama wala akina baba. Mimi nimewaambia, leo naenda kuwachafua Bungeni, naenda kusema ukweli Bungeni, mmezidi nyie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anakusanya fedha, huwezi ukamtuma mtoto wako akutekee maji kwa kutumia msege. Akutekee maji kwa kupitia msege au kajungio, maji hayawezi kufika. Sasa ni baadhi ya Wabunge hawa, ni sawa na msege, sawa na chujio la kuchujia chai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama ndiyo mhimili wako, sisi ni mhimili, lazima tuchunguze safari za Wabunge kwa michezo wanapokwenda nje. Watatuletea aibu kubwa, kwa sababu huwezi kwenda kucheza mpira huna mazoezi; huwezi kuvuta kamba huna mazoezi; au kucheza netball bila mazoezi. Hii lazima tuchunguzane ndugu zangu. Siyo tunapiga kelele hatuna maji, hatuna barabara, hatuna umeme wakati nyie mnatanua, mnakwenda kustarehe huko. Hamna faida yoyote kwenda nje. (Makofi)

(Hapa, baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachangia sasa. Mheshimiwa Waziri nisikie vizuri, wewe umetoka katika Mkoa wa Kigoma. Mkoa wa Kigoma umepakana na DRC Congo. Katika nchi tajiri katika ukanda wetu ni DRC Congo. Lazima akili yako, macho yako, Wizara yko ielekeze kufanya biashara na DRC Congo kupitia Ziwa Tanganyika. Lazima tuunde meli pale kubwa ya kupakia ma-container kupeleka Miji ya Kalemii, Uvira, Moba na Bujumbura kupitia reli ya kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya nyuma enzi ya Mwalimu Nyerere tulikuwa na meli ya mafuta pale, inapeleka mpaka Zambia kupitia Bandari ya Kigoma, leo hakuna kitu. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri, yeye anatoka Kigoma, anafahamu kabisa, DRC Congo mzee ndiyo nchi pekee tajiri katika ukanda huu wa kwetu na ina watu wengi na kila kitu. Tushirikiane na DRC Congo, ukikaa chini ya uaridi utanukia kidogo. Utafanya na masikini mwenzako, utapata kitu gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima akili yetu ielekee DRC Congo kufanya biashara nao. Tusidanganyane hapa, Congo ndiyo pekee inayoweza kutuokoa. Leo nasikia kuna ujumbe mkubwa toka DRC Congo uko Uganda kule, wafanyabiashara wa DRC Congo. Nasi tuelekeze nguvu zetu kule, itatuokoa ile nchiā€¦

MWENYEKITI: Wanataka kujenga barabara ya kilometa 1,000 kutoka Uganda kwenda DRC Congo. Uko sahihi Mheshimiwa, endelea.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, tujitahidi. Vilevile wafanyabiashara wetu wote, leo wanachukua ma-container China, biashara ni China. Cha ajabu kule China kabla hujatoa container kuna inspection, unaacha dola 1,000 kukagua eti bidhaa zao. Wakati wanatengeneza wenyewe! Ukifika Dar es Salaam tena, TBS wanakagua ile bidhaa, wanalipa dola 1,000 kule. Sasa sijui kama Wizara ya Fedha inafahamu hiyo dola 1,000, inarudi ngapi katika nchi yetu? Inachukuliwa China yote, kwa maslahi gani wakati tunanunua bidhaa kutoka China zao wenyewe, ulipie container? Ma-container mangapi kwa mwezi yanakuja Dar es Salaam? Tunapoteza shilingi ngapi? Dola ngapi tunapoteza kwa kila container kwa ma- container yanayoingia nchini kwetu kutoka China?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila container, uliza vijana wafanyabiashara wa Kariakoo, lazima waache dola 1,000 wanaita inspection kule China. Ukifika Dar es Salaam, lazima hilo container tena TBS wachukue pesa. Sasa tutafanyaje biashara, wanatuchukulia dola 1,000 Wachina kila container, wakati tunanunua bidhaa zao wenyewe? Je, kama hiyo dola inakuja kwetu Tanzania, tunajuaje kama inakuja yote dola 1,000 kwetu Tanzania? Lazima tuwe macho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukaguzi wa ma-container nimeshamwambia Mheshimiwa Waziri, lazima nipate majibu haraka sana kuhusu hiyo, kama wanakagua ma-container yetu au namna gani. Kuhusu Bandari ya Kigoma, imekufa, haina maslahi kabisa, imekufa Bandari ya Kigoma. Ukifika pale wanakula tu mishahara. Lazima tuifufue kwa ajili ya kusaidia kwenda Bujumbura na Kalemii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani ni kitu cha ajabu kusema kweli, tunaacha hela. Sisi bandari yetu tumezungukwa na nchi, tumezungukwa na Zambia, Malawi, Burundi na Rwanda. Akili yetu yote kwa sasa tuhakikishe bidhaa zote za kwenda Malawi, Zambia, Mashariki ya DRC Congo, Burundi na Rwanda zinapitia katika nchi yetu. Lazima akili yetu ilenge hapo. Akili yetu ilenge bidhaa zote za kwenda Rwanda, Burundi, Mashariki DRC Congo, Zambia na Malawi, lazima zipitie kwenye bandari zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Tunduma pale lazima tufanye mikakati kupanua barabara. Msongamano wa magari ya pale Tunduma lazima tuupunguze ili biashara iende haraka haraka pale Tunduma, siyo gari inakaa siku tano, siku sita au saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fanya ziara, nenda pale Tunduma, utaona huruma. Magari yanalala mpaka 1,000 au 1,500. Sasa hii biashara mzee, nchi lazima tuwaze biashara. Haiwezekani kuweka magari mpaka 1,000 pale Tunduma kwa muda mrefu. Kuna malori ya mafuta, ukitokea moto pale Tunduma, mji mzima utaungua. Mji mzima wa Tunduma utakwisha. Malori yanayojaa Tunduma pale ni ya ajabu, msongamano ni wa ajabu, kwa nini msifanye taratibu za kuvusha magari haraka haraka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtafute mpaka mwingine kutoka nje ya Tunduma kule yapite magari, custom waongeze, tupate hela haraka haraka, tunakawaiza biashara. Ndiyo maana sisi Watanzania ukiambiwa saa 3.00 uje unakuja saa 5.00; ukiambiwa uje saa 6.00 unakuja saa 9.00. Hatuendi namna hiyo. Ukiambiwa saa 6.00 iwe saa 6.00. Kama hujafika saa 6.00 unaachwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuamke tufanye biashara. Sasa ni kipindi cha kufanya biashara. Tumwige Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli anataka mambo ya papo kwa papo. Aliyofanya Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli hakuna mtu aliyetegemea, miradi hii ya kujenga reli ya mwendokasi, mambo ya umeme nani alitegemea? Kununua ndege haraka haraka, nani alitegemea? Inataka uamuzi wa ujasiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashangaa, unatamka kabisa wewe mkuu wa chama kabisa mwenyekiti wa chama au katibu wa chama unamuhusisha Rais Magufuli na uchaguzi wa Serikali za Mitaa wakati kila siku kwenye redio na television Rais anahamasisha wananchi chagueni kiongozi yeyote akiwa wa CCM akiwa CHADEMA, ACT Wazalendo chagueni; anatamka mwenye Mheshimiwa Rais;leo utamsingiziaje Rais anaingia kwenye mchakato wa uchaguzi, anahusika wapi?Pambaneni na Tume ya Uchaguzi, hamasisheni wenyewe huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wenyewe wameshachoka,kazi anayofanya Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli inaonekana, sasa mgombea gani atakwenda kugombea kwenye chama kingine aonekane? Wenyewe walikuwa wanadai ufisadi amepigana na ufisadi amemaliza, amewabana watu wote, amefungua mahakama ya ufisadi. Kila kitu walichokuwa wanadai kwenye mikutano ya hadhara Mheshimiwa Rais katanguliza mbele; sasa hawana hoja, hakuna hoja.

Mheshimiwa Spik, jana Mheshimiwa Waziri Jafo kawaambia, jamani hamna kuweka mpira kwapani, wote nendeni kwenye uchaguzi. Sasa mnataka kudai tume huru hiyo tume huru utaitoa wapi?Mbinguni kwa malaika? si binadamu wetu hawa hawa? Kwahiyo ndugu zangu hakuna haja ya kubabaika, tarehe 24 twendeni kwenye uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sehemu zingine kama kule Nkasi chama kama cha CUF wala hukisikii kabisaa!Wala hatukijui kabisaa!Sasa nashangaa unasimama hapa unasema fomu zetu sijui umetunyima sijui zimefanya namna gani; nani anayekufahamu? nani anakujua?Ni mambo ya miujiza kabisa.

Ndugu zangu tusisingiziane mengi twendeni kwenye uchaguzi. Mambo yalijionesha mapema kabisa; madiwani wangapi wamehama, inajulinana, Wabunge wangapi wamehama, wenyeviti wangapi waliacha kazi. Sasa ninyi wenyewe mnavyojiona na mnavyojipima mmeona hamna hoja. Mmebaki wachache ndugu zangu, mti unaokauka hata ukiumwagia maji mizizi imeshakauka, hauwezi kustawi

MHE. MCH. PETER S. MSINGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa

SPIKA: Mchungaji unamnyanyukia Mheshimiwa Keissy?

MHE. MCH. PETER S. MSINGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka nimpe taarifa tu.

T A A R I F A

SPIKA: Haya mpe taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSINGWA: Mzungumzaji anayezungumza kwamba kuna vyama vingine havipo kwenye maeneo yake; inawezekana kweli vyama vingine havipo kwenye maeneo yake lakini vyama vingine vipo. Isipokuwa nataka nimjulishe kwamba malalamiko ambayo wengine wanayatoa hapa; mfano mzuri ni mimi mwenye pale Jimboni kwangu Kata ya Gangilonga tangu siku ya kuchukua fomu ilifungwa mpaka mwisho mtendaji anaondoka; haijawahi kuchukuliwa fomu hata moja, hayo ndiyo malalamiko nilitaka apate taarifa; na maeneo mengine ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachosema, hatukimbii uchaguzi tunataka tuwe na uwanja fair.

SPIKA: Mheshimiwa Keissy unaipokea taarifa hiyo?

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa, siipokei taarifamaana clipya Mheshimiwa ninayo. Alipokwenda Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli kule kwake Iringa alimsifu vibaya. Kwamba nakushukuru Mheshimiwa Rais miradi yote naiona Mheshimiwa Rais, kwahiyo sisi hatuna tatizo lolote. Clip yako tunayo Mheshimiwa na inatembea Mheshimiwa; wewe mwenyewe Mheshimiwa ulimpongeza Mheshimiwa Rais kwa hali na mali ulimpongeza Mheshimiwa sasa sijui kama wananchi wako watakuelewaje Mheshimiwa

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

T A A R I F A

SPIKA: Mheshimiwa Daniel Nsanzugwanko nimekuona, taarifa.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu kumpa taarifa ndugu yangu Keissy, na mimi nakubaliana naye, kwamba kwa mfano Jimbo la Kakonko yule aliyekuwa mpinzani mkubwa wa Chiza kwenye by-election na timu yake yote wamerudi CCM leo. Kwahiyo ni kweli hawana wagombea. Nilitaka tu uwe na amani katika jambo hilo.

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Keissy muda umeisha.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa, anayosema unaona anayadhihirisha kabisa napokea taarifa Mheshimiwa Msigwa mwenyewe clip yake inatembea kabisa anaiona; sijui kama alikuwa si Msigwa huyu au namna gani, kavaa hivi hivi kila kitu na suti. Sasa nadhani clip yake labda nitamkumbusha, nitakutumia clip in box, labda utaisikiliza vizuri. Wewe mwenyewe ulikiri kwamba awamu ya nne imefanyakazi.

SPIKA: Awamu ya tano.

MHE. ALLY K. MOHAMED: Awamu ya tano imefanyakazi nzito. Jana nililala Iringa kwa Mheshimiwa hapa, hata uchaguzi watu wamesharidhika, watu wamesharidhika Mheshimiwa Msigwa umebaki peke yako, usione aibu kurudi Mheshimiwa Msigwa rudi haraka tunakuhitaji. Ahsante sana nashukuru sana. (Makofi/ Vigelegele)