Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niweze kuchangia kwenye mpango huu wa maendeleo, napenda kumpa pongezi kwanza Mheshimiwa Rais kwa mambo mazuri aliyeyafanya na anaendelea kuyafanya hasa kwenye miradi yote ambayo inatekeleza na ambayo imeshatekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake na watendaji wote kwa mambo mazuri kutuletea huu mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuongelea kwenye mambo ya vipaumbele hasa vinavyowagusa wananchi nikianza na kilimo, kilimo kama tulivyosema kina ajiri asilimia 65 ya wananchi na kimekuwa kwa asilimia 5.3 na kinachangia pato la Taifa kwa asilimia 28. Licha ya hivyo nilikuwa naomba huu mpango tukiweza kuondoa umasikini hasa kwa watanzania naona kilimo kiweze kiweza kipaumbele kwa sababu wananchi wengi tunaona kuwa wanaajiriwa pamoja na kilimo. Kwa upande wa kilimo hasa kuna utata wa afisa ugani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nashauri kuwa tuelekeze kwenye mpango wetu huu kutumia TEHAMA kutokana na tatizo hili tutumie TEHAMA hasa kwenye simu zetu kwa kuwafikia wakulima kuwapa ushauri kutokana na TEHAMA tunaweza tukafikia wakulima wengi, hii teknoloji tayari imeanza kutumika kama kwa kuanzia kufuatana na NGO’s mbalimba na taasisi mbalimbali na watafiti na imeonekana kuwa inafaa. Kwa hiyo, kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo Mheshimiwa Dkt. Mpango naomba tuangalie jinsi ya kuwekeza kwenye kilimo na kwa kutumia IT hasa kuwafikia wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nikisema kilimo kuwa kinapunguza umasikini siyo kilimo cha kawaida ninyi mnajua ni mashahidi mmeona kuwa mabadiliko ya tabia nchi. Kwa hiyo, naomba huu mpango uwekeze sana kwenye kilimo cha umwangiliaji tukiwekea kwenye kilimo cha umwangiliaji tutakuwa na uhakika kuwa tutawasaidia wakulima wengi kutokana na kilimo kwa sababu wakulima wengi wanalima mambo haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ambalo nilikuwa nataka kuongelea kuhusu kilimo ni kuwa hatujawekeza sana kwenye uvuvi wa bahari kuu kwenye upande wa uvuvi naomba huu mpango safari hii ujiwekeze na kujielekeza sana kwenye uvuvi wa bahari kuu na hii iendane pamoja na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi kwa sababu ukiangalia hatuna viwanda vingi vya kuchakata mazao ya uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye ufugaji, kwenye upande wa ufugaji tunafuga ndiyo lakini huu mpango uangalie licha ya kuwa na mifugo mingi lakini hatuna viwanda hasa vya kuchakata mazao ya ndani hasa kama maziwa mnaona mpaka sasa hivi viwanda vya maziwa ni vichache sana na bado tuna import maziwa ya unga kuja kufanya maziwa fresh kwahiyo nilikuwa naona huu mpango uweze kuwekeza kwenye viwanda vya ndani ambavyo vitaweza kuchakata mazao yetu ya kilimo uvuvi pamoja na ufugaji na hasa hasa ni kimaanisha kwenye upande wa viwanda vya maziwa na matunda na mafuta kwa mfano unaona hatuna viwanda vingi vya mafuta ninyi nyote ni mashahidi mnaona mafuta yanakaakaa barabara yana grow rancidity yanafanya nini kwa hiyo nilikuwa nashauri kuwa tuweze kupata uwekeze kwenye viwanda kusudi tuweze kufufua na kuendeleza viwanda ambavyo vinastahili kwa mazao yetu ya ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine kinachogusa kwa upande wa mpango ni maji upande wa maji naona kweli Wizara inafanya vizuri sana lakini mpaka sasa hivi wananchi wote hawajapata maji tukitaka kwenda vizuri kwenye mpango huu wa 2020/2021 naomba sana tuwekeze sana kwenye maji kwa sababu wananchi wote waweze kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ni asilimia 64 tu vijijini na asilimia 80 mijini kwa hiyo mwaka ni kesho 2020 tuweze kupata maji ya kutosha angalau vijiji vyote viweze kupata maji ya kutosha. Hivyo hivyo nakwenda pamoja na umeme, umeme nashukuru mawaziri mnafanya vizuri sana kwa upande wa nishati, lakini naomba vile mpango na wenyewe huu mpango uweze kujikita usiache umeme ingawaje wanafanya vizuri hasa tuweze kuona kufikia vijiji vyate kwenye umeme kusudi twende vizuri kwenye umeme na wananchi wote waweze kupata umeme ingawaje wanafanya vizuri naomba tusivisahau.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ninalopenda kuongelea haraka haraka TARURA inafanya vizuri lakini kama wenzangu walivyosema ni kweli wanapewa asilimia kidogo asilimia 30 haiwezi kutoza barabara zote za mjini za TARURA na barabara za vijijini zinazoendeshwa na TARURA na hasa barabara za mashambani kwahiyo naomba huu mpango uweze kuelekeza kwenye mambo haya na wenyewe waweze kupata fungu zuri kwenye mpango wetu huu tunaokwenda nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuongea hayo naomba kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais tena na tena kwa Standard Gauge kwa sababu sasa hivi inakwenda kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro asilimia 63 na kuendelea mpaka kutoka Makutopola kuendelea ningependa iweze kufikia mwanza pamoja na Kigoma iende haraka kusudi barabara zetu ziache kuharibika barabara zetu zinaaribika kwa sababu lori. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa mfano tukipata hii ikaisha itaweza kusafirisha mizigo na barabara zetu zitaendelea kuwa nzuri kwa hiyo huu mpango unawenyewe ujielekeze huko tuone jinsi tutakavyomaliza na pongezi nyingine natoa kwa bwawa la Nyerere nasema ahsante sana naamini wananchi wote likiisha wataweza kupata umeme wa kutosha kwa hiyo, na hapo hapo nasema Mpango wa ardhi waweze kuangali mpango wa ardhi kwa sababu kuna mambo ya utalii hapo na kuna mambo ya kilimo cha umwangiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba kupongeza kwa kutupatia Halmashauri pale Morogoro kutupatia Halmashauri ya Kilombelo pamoja na Halmashauri ya Mlimba naamini mambo yatakwenda vizuri na sisi nikiwa Mbunge wa viti maalum naamini tutafanya kazi nzuri kwenye halmashauri hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru ahsante sana na Mwenyezi Mungu akubariki naunga mkono hoja. (Makofi)