Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi hii awali ya yote kabisa naomba kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ambaye amenijalia uzima na kuweza kusimama kuchangia hoja iliyopo mbele yetu siku ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba pia nimpongeze ni join wenzangu kumpongeza sana Waziri wa Fedha na Naibu wake Dkt. Mpango na Dkt. Ashatu kwa kazi kubwa nzito na nzuri wanayoifanyia wizara hii ya fedha ambayo kusema ukweli ndiyo uti mgongo wa mpango ambao tunautengeneza kuweza kuinua uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nichangie maeneo matatu eneo la kwanza ni katika pato la Taifa katika uchambuzi ambao tuliufanya kama Kamati ya Bajeti, niko kwenye kamati hiyo tuliona kwamba takwimu hizi tulizochambua za mwaka 2016, 2017/2018 pato letu la Taifa lilikuwa kwa asilimia saba hadi 7.2 na katika miaka yote hii tofauti ni asilimia 0.1.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tukitizama matarajio ambayo tunayaweka mwaka 2020/2021 tunatarajia kwamba tutakuza pato letu la Taifa kwa asilimia 10 sasa tunajiuliza hizi takwimu za ukuwaji wa pato la taifa katika jinsi ilivyoainishwa imeweza kukuwa kwa ajili ya nini, kwa ajili ya uwekezaji upi ambao umewekwa na Serikali hadi pato letu limekuwa kwa kiasi hicho na tutakuza sekta hipi ama tutawekeza sekta zipi ili tuweze kufika asilimia 10 mwaka 2020/2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchambua takwimu hizo tumeona kwamba sekta ambayo haikuwezeshwa vizuri ni sekta ya kilimo, lakini tukiendelea kuchambua tunaona kwamba pamoja na uwezeshwaji duni wa sekta ya kilimo imechangia pato la Taifa kwa asilimia 28.2. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa najiuliza hivi ukuwaji wa sekta ya kilimo ya asilimia 3 kwa mwaka na inachangia pato kwa asilimia 28.2 je, Serikali ikawekeza kwa hali ya juu katika sekta ya kilimo tutaweza kufikisha asilimia ngapi ya pato la Taifa, ni wazi kama itakuwa kwa asilimia zaidi ya zaidi ya tatu sasa kwa mfano sita au saba itachangia pato letu kwa asilimia zaidi ya 70. Kwa hiyo, hii ina justified ni kwanini Wabunge wengi na sisi na mimi mmoja wapo kwamba tunataka Serikali iwekeze kwa nguvu sana kwenye sekta ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasema hivyo kwa sababu sekta ya kilimo ndiyo inaajiri watu wengi na tunaposema pato la Taifa ni asilimia 10 basi haieleweke vizuri kama bado kwenye mifuko ya watanzania hakutakuwa na chochote watu watakuwa bado maskini, lakini tukikuza sekta hii ni wazi itafungamanisha pato la Taifa ukuwaji wake pamoja na maendeleo ya watu na kuondoa umasikini, lakini vile vile, kwa sababu ina ajiri watu wengi inaweza pia kupunguza mfumuko wa bei. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naungana na wenzangu wengi ambao wanaunga mkono kuwekeza zaidi katika sekta ya kilimo kwa manufaa ambayo tumeitaja hapa kwamba kusema kweli tunataka kufungamanisha pato la Taifa na maendeleo ya watu wetu, watu watakuwa na hela mfukoni na umasikini wa kipato utapungua mara dufu na hivyo kujiza uchumi na wananchi wetu watasonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukuzaji wa sekta ya kilimo ambapo tunaambiwa kwamba sekta hii inajumuisha sekta ya mifugo na uvuvi ni wazi basi tutakapokuza sekta hii ama tutakapo wekeza kwenye kilimo sitaki kuingia details kwa sababu Waheshimiwa wengi wameizungumzia na kueleza kwamba tukuze hasa tulenge mazao gani na hapa na pale. Lakini kusema kweli naungana na wenzangu na ninaomba Waziri aweze kutuwainishia katika mwongozo wa mpango tunaoelekea kuutengeneza wa 2020/21 ni mikakati ipi mizuri ya kuwezesha sekta ya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ni sekta ya Benki ambayo nataka kuchangia kwa kifupi sana vilevile, uchambuzi wa kamati unaonyesha kwamba Ma benki yetu sasa hivi yanaukwasi mkubwa sana sasa tunajiuliza kama benki zinaukwasi na hatuna tatizo ni suala la kuelekwamba ni kwanini sasa bank zinakuwa na ukwasi wakati tunatarajia kwamba pengine ukuaji wa sekta ya benki ni pale ambapo benki zinatoa mikopo unaweza kukuza wigo na kupanuka na kukuza uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili kidogo halijaeleweka kwahiyo tutaomba Mheshimiwa Waziri atueleze ni kwanini kuna ukwasi mkubwa liquidity ya fedha katika benki zetu kiasi ya ziada kiasi ambacho kinatarajiwa kwa sababu tunajuwa kwamba ukuwaji wa sekta ya benki ni kule ambapo inatoa mikopo tumeelezwa katika taarifa kwamba pengine sababu ni sekta za benki kuogopa kukopesha kwa kukwepa mikopo chechefu, lakini bado si sababu za kutosheleza. Nadhani ni vizuri kuangaza macho zaidi Mheshimiwa Waziri katika sekta hiyo ili iweze kukaribisha sekta binafsi waweze kukopa na hata watanzania wenye uwezo kuweza kuwekeza na kuweza kuendeleza miradi ya maendeleo kwa kutumia fedha za benki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika eneo hili nilitaka kuzungumzia riba benki, kwa miaka mingi tumekuwa tukilalamika kwamba riba inayowekwa na benki kwenye amana za wateja tunapoenda kukopa ni kiwango kikubwa sana asilimia 16 na kuendelea lakini unapowekeza fedha zako benki unawekewa riba ndogo sana ya asilimia 3 sasa najiuliza, kwa sababu nafanya kidogo ukobeshaji kwa wanawake maskini kwa hiyo, najuwa kidogo suala la ukopeshaji siendi kwenye kiwango cha benki lakini najuwa riba unapoweka katika amana za mteja unaziweka kama cost borrowing kwa mfano gharama ile ambayo una incur wakati unakopesha.

Mhesimiwa Mwenyekiti, sasa gharama ya kukopesha kwa sekta ya benki kwa mfano sisi Wabunge tukikopa benki hivi wanapata gharama hipi wanangoja tu wamekaa mezani wanachukuwa installment zile ambazo zinakatwa kwenye mishahara yetu ama hata wakopaji kutoka nje ya Bunge wanaokopa benki incur gharama yoyote kulinganisha na mteja gharama anayo incur katika kutafuta mkopo wa benki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tulikuwa tunaomba kwa kweli suala la riba ya benki kuwa kubwa kwenye amana za wateja ni suala limepigiwa kelele kwa miaka mingi kwa hivyo tulikuwa tunaomba hili nalo liangaliwe sasa kama Serikali tunaweza tukapiga kelele miaka nenda rudi lakini hakuna kinachofanyika asilimia 16 na zaidi kulinganisha na asilimia tatu ni kiwango cha tofauti ya asilimia 13 huo ni kama unyonyaji kwenye fedha za wateja. Kwa hiyo, eneo hilo nalo liweze kuangalia kuboreshwa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa kengele ya pili imelia.