Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, napenda niungane na wenzangu wote kwanza kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha, Naibu Waziri wa Fedha, pamoja na timu yote ambayo wameandaa Mpango huu vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yawezekana hapa tuna ongea lugha ambayo haieleweki tu, lakini Watanzania sasa wanaelewa, hata Mheshimiwa ambaye amemaliza kuzungumza sasa hivi anasema kwamba eti kwamba tunaua demokrasia, demokrasia ni historia katika nchi yoyote ile, Watanzania sasa hivi naomba niwapeleke kwa statistics.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia mwaka 2015/2016 Uwekezaji kwa wananchi ilikuwa ni zaidi ya trilioni 29.5 .

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016/2017 ukafika trilioni 48.5, 2017/2018 trilioni 55.17, na sasa hivi hadi Juni 2019 ni trilioni 59. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii maana yake nini, translation yake Mheshimiwa ambaye alikuwa anazungumza hapa ni kwamba Watanzania sasa wameanza kuelewa demokrasia ni maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Watanzania wameelewa kwamba kupitia maendeleo haya sasa walichagua Serikali halali ya chama cha halali na ndiyo maana sasa hivi hata wagombea wengi hawajajitokeza kwa sababu hiyo. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Eehhe!

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua tuseme kitu ambacho Watanzania wanataka, hatutaki maneno na porojo, tunataka translation ya uchumi katika maisha ya Mtanzania, na sasa hivi nchi inavyokwenda chini Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ndani ya miaka minne, tumeona mambo mengi yamefanyika na ndiyo watu walikuwa wanahitaji hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo, mnaposema kwamba hakuna demokrasia, jamani, hivi demokrasia maana yake nini? Demokrasia ni kwa ajili ya watu, ni kwa ajili ya watu na kwa mahitaji ya watu, sasa leo Watanzania wameridhika na maendeleo yanayoendelea sasa hivi hapa nchini, tumesema ujenzi wa misingi ya uchumi. (Makofi)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MBUNGE FULANI: Taarifa ya nini wewe….

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Chegeni kuna taarifa. Mheshimiwa Frank Mwakajoka.

T A A R I F A

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpa taarifa mzungumzaji anasema wananchi wameridhika na ndiyo maana hawajajitokeza, lakini tunataka tumkumbushe tu kwamba sisi tumesimamisha vitongoji vyote, Mitaa yote na Vijiji vyote nchi nzima, lakini pia hatutaki demokrasia anayosema kama ile ambayo walikuwa wananyang’anyana matokea na Mheshimiwa Kamani. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji demokrasia ya haki ambayo Mtanzania anataka kwenda kupiga kura, ahsante. (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Dkt. Chegeni unaipokea taarifa hiyo?

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naona siipokei. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu nazungumzia hapa ni maendeleo ya Watanzania. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba leo hii, kama umewekeza kwa kiwango hicho, maana yake ni kwamba Watanzania walichokitamani wanakipata, leo ukizungumzia suala la maendeleo, tunazungumzia katika Mpango huu kwamba lazima tujenge misingi ya uchumi wa viwanda, maana yake nini, maana yake kwamba tujielekeze Watanzania sasa kumboresha Mtanzania na aweze kufikia kiwango cha kujenga uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tupunguze porojo na maneno, Watanzania tumeongea sana, miaka nenda rudi, lakini ndani ya minne, tumefanya mambo makubwa sana, ambayo kila mmoja ana historia nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ninyi Wabunge wote, pamoja na mimi tukienda Majimboni kwetu tunaona miundombinu iliyopo, hii ya Afya, Elimu, Maji, Barabara na vyote vile, ni kwa sababu gani kumekuwa na usimamizi mzuri wa utekelezaji wa Mipango ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wananchi wanachagua nini, wanachagua maendeleo, hawachagui maneno, Watanzania wanachagua maendeleo, sasa mnapoanza kulalamika kwamba hakuna demokrasia, nawashangaa wakati mwingine, hebu muanzie nyumbani kwenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mna demokrasia gani? Kwa sababu katika baadhi ya vyama hapa hakuna demokrasia ndani ya vyama vyenu, lakini hamlalamiki, sasa niseme kwamba hebu tuji-focus kwenye Mpango wa maendeleo ambao una tija zaidi kwa Watanzania.

MBUNGE FULANI: Una demokrasia!

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mpango huu ukiangalia mwaka huu peke yake wa fedha tumetenga asilimia 37 ya Bajeti yote kwa shughuli za maendeleo, hao ni Watanzania wanataka hayo, leo umepanga trilioni 12.2 kwa ajili ya Miradi ya maendeleo, na hii ni kwa Watanzania wote bila kujali wa chama gani, na maendeleo hayana chama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu-translate ndoto ya Mheshimiwa Rais na hii naomba Watendaji na Wasaidizi wote, ndoto ya Mheshimiwa Rais kutokana na Watanzania sasa wanapata maisha bora, wanapata maendeleo ya kiuchumi, wanasonga mbele, haya yote utayafanya ikiwa sisi sote tutaenda katika mwendo ule ambao Mheshimiwa Rais anautazama, na mimi niseme kwamba lazima tufike Watanzania tujifunze tufanye namna hiyo, lakini vilevile Miradi ya Mikakati ambayo leo Watanzania tunaifanya, tumeona Miradi mbalimbali haijafanyika, lakini tumeanzisha Miradi mikubwa ambayo hatukuwa nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa na Mashirika mengi ya Umma, tuliweza, na mengine yalikufa, mengine hayakufanya vizuri, leo hii kupitia Wizara ya fedha, kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina na Kamati ya Uwekezaji tumeweka vigezo, KPI ili kusudi uweze kupima mwenendo wa kila Shirika na Taasisi ya Serikali aidha inatoa huduma au inafanya biashara, na lengo lake ni kwamba tuongeze mapato katika mapato yasiyotokana na Kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa kwamba Watanzania tukiimba wimbo mmoja tutafika safari yetu tunayoitaka, lakini tukienda kwa safari hii ambayo kila mmoja anataka aimbe anavyotaka mwenyewe tutashindwa kufika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tuangalie, naomba tuangalie kwamba tunapaswa tujenge kesho, kesho iliyo bora kwa Watanzania, unaijengaje kesho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kuijenga kupitia Miradi ambayo lazima Watanzania tuisimamie, lakini katika Mpango huu naomba tu Mheshimiwa Waziri wa Fedha naomba tujipange kidogo, hasa kwa Wakulima, Mkulima analima zao lake akijua kwamba akishavuna aweze kuuza, na ndiyo maana ya kuweka mnyororo wa thamani, lakini vilevile kumfanya Mkulima apate tija na Kilimo chake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mkulima anapolima na ningeomba sana liingie hili katika Mpango unaokuja, Mkulima anapolima awe na hakika ya kupata bei ya mazao yake ili hii Mkulima imtie moyo wa kuweza kuzalisha zaidi na tuongeze tija katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mkulima wa pamba ameuza pamba toka mwezi wa tano mpaka leo hii hajalipwa pesa yake, halafu unataka mwaka aanze kufanya Kilimo tena kwa ajili ya mwaka kesho, hii si dalili njema, ninaomba sana wasimamizi ndani ya Serikali lisimamieni hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajua kuna suala la soko huria lakini kama Serikali lazima itoe guarantee kwa Mkulima huyu au mazao yote, iwe ni Pamba, Korosho, Katani, Chai na mazao mengine yote ili Mkulima apate tija kile ambacho anataka kukizalisha, lakini pili Viwanda hivi vitajiendeleza namna gani. Lazima na guarantee ya mazao yanayotokana na Kilimo chetu, lazima tufungamanishe sasa ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo lazima tulifanye kwa nguvu zote kwamba sasa hivi Mtanzania yule yule afungamanishwe na maendeleo ili aweze kupata maisha ambayo tunayohitaji, leo hii mkulima tumemsaidia sana kumwekea miundombinu ya barabara, umeme, maji, upande wa afya, sekta ya afya, upande wa elimu, Serikali inatoa fedha nyingi kila mwaka, lakini yote haya sasa lazima yasimamiwe vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha, mwanzoni nilikuwa sikuelewi elewi, lakini nimeanza kwamba sasa kumbe wewe ni msimamizi mzuri sana wa raslimali za Watanzania na ni mzalendo, na hata Katibu Mkuu wako wa Fedha na Naibu wa Waziri wako kweli mnafanya ya kizalendo. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mwambie shikamoo…

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, na ninaambiwa hapa niseme shikamoo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha, nakwambia hapa niseme shikamoo Mheshimiwa Waziri wa Fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumzia Ofisi ya Msajili wa Hazina, endelea kuimarisha, inachangia pato lisilotokana na kodi zaidi ya shilingi trilioni moja sasa hivi kwa mwaka. Ninaomba iwe ni ofisi ambayo inapewa kila aina ya support kusudi itekeleze majukumu yake inavyotakiwa.

Mheshmiwa Mwenyekiti, vilevile Taasisi za Serikali na Mashirika ya Umma, yafuate misingi ambayo imewekwa na kufanya hivyo nina imani tutaweza kufufua uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwa kusema kwamba Watanzania tunaanza kumwelewa Mheshimiwa Rais, tuendelee kumwelewa. Makandokando mengine haya, naomba Watanzania tupate fursa ya kuyazunguza, lakini kama ni Mpango, tuuzungumzie Mpango kwa malengo na maslahi mapana ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na ninaunga mkono hoja hii. (Makofi)