Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. PROF. NORMAN A. S. KING: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kumpongeza Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa Mpango mzuri waliouleta. Hawa ni rafiki zangu na wameleta Mpango mzuri sana, nawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, nampongeza sana Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi kubwa na nzuri ambayo imemfanya apate sifa Afrika na dunia nzima ya kuekeleza na kusimamia mipango ya maendeleo yetu wenyewe kwa fedha zetu wenyewe. Mipango ya ujenzi wa bandari, viwanja vya ndege, maji Mtwara na mipango mingi mizuri inayofanywa na Rais wetu, inampa sifa na heshimia duniani kote. Mungu ambariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie kidogo maeneo machache. Unapoongelea kukuza Pato la Taifa ni vizuri kuangalia katika sura mbili. Sura ya kwanza ni ile inayomgusa mtu mwenyewe mmoja mmoja, fedha inayomgusa mtu mmoja mmoja. Kwa hiyo, naomba sana kwenye eneo hili, benki zetu hizi za kilimo kama Tanzania Investment Bank tuweke riba ndogo sana kwa wakopaji wanaomaanisha kwenda kuwekeza kwenye kilimo angalau asilimia 10 lakini sio 17 au 19, haifai kwa sababu ni kilimo. Kwa hiyo, naomba sana wawekezaji wa kilimo wanapokwenda kukopa Tanzania Investment Bank wakope kwa asilimia angalau 10. Tukifanya hivyo basi tutaona maparachichi yakipandwa kwa wingi kule kwetu Makete, Rungwe na kila sehemu yatapandwa kwa wingi kwa sababu ukopaji utakuwa umerahisishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni dhahabu yetu. Kwa sisi wachimbaji wadogo wa dhahabu ni vizuri sana Geological Survey Institute inayoongozwa na Profesa Mruma ikapewa fedha kwenda kufanya explosion test ili tuwe na uokaji wa dhahabu tunayoijua kiwango chake. Geological Survey Institute inayongozwa na Profesa Mruma ipewe fedha ili kwenda kufanya kazi hizo za kuhakiki kiwango cha dhahabu kilichopo kwenye ardhi kwa kila mchimbaji wa dhahbu mdogo mdogo. Tukifanya hivyo, tutasaidia wananchi walio wengi kupata dhahabu yao na fedha zao kwa wingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni upande wa elimu. Kwa mfano, shule za msingi Makete ni wastani wa walimu watatu kila shule sasa wanafunzi hao watasomaje? Naomba sana Wizara ipeleke walimu wa sekondari kwa mshahara wa sekondari wakafundishe shule za msingi, wale waliomaliza wapelekwe shule za msingi kwa mshahara wa sekondari. Wanachotaka wao ni fedha (mshahara), wapelekwe kwa mshahara wa sekondari lakini wafundishe shule za msingi. Shule za msingi orientation yake ni ndogo, figisu figisu na michanganuo ya kusema kwamba ufanye hivi, ufanye hivi, wanapewa elimu ya mwezi mmoja, wanahamasika halafu tunajenga shule zetu vizuri kwa sababu sasa hivi ni tatizo kubwa sana kwa shule za msingi za elimu wilayani Makete. Walimu watatu ndiyo wastani wa walimu kwa shule zangu, hali ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, nihitimishe kwa kusema kwamba kama mipango yote hii tukiifanya, upande wa elimu tukawapeleka walimu wengi katika shule za msingi, upande wa kilimo tukawapa wakulima mikopo ya asilimia ndogo, asilimia 10 kwa mfano, Upande wa dhahabu tukapeleka fedha Geological Survey kwa Profesa Mruma akaweza kuhakika kiwango cha dhahabu kila sehemu basi tutakuwa tumesaidia kukuza uchumi wa nchi hii. Nafahamu kwamba Geological Survey team walikuwa wameshapewa fedha kwa ajili ya kufanya kazi hiyo, sasa hivi hazipo lakini walikuwa wameshapewa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho nizungumzie kuhusu ujenzi wa reli. Ujenzi wa reli ni jambo muhimu sana lakini naomba sana, reli ninayoikazia hapa ni ya Uvinza - Msongati, kwa sababu Msongati kuna chuma tani zaidi ya 3,000,000. Watazamaji wote wa reli hii wanafikiria kwamba ile reli itakuwa inameza chuma kile kwa kusomba chuma kile ili tonnage yetu iwe ya maana. Tonnage inayopelekwa Mwanza na Bakhresa ambaye ndiye mpelekaji mkubwa, akipeleka mara moja tu Uganda tonnage yake yote itakuwa imeisha, meli imeenda mara moja inakuwa imeisha lakini tonnage ambayo ni ya uhakika ni ya Msongati kwa sababu pale pana chuma na tayari tunao mkataba walioingia Mawaziri waliopita wa Burundi na Tanzania wa jinsi ya kushirikiana na DRC-Congo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mungu awabariki sana, ahsante sana, naunga mkono hoja. (Makofi)