Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii nami niweze kuchangia mpango ulioko mbele yetu. Nianze tu kwa kuipongeza Serikali na sisi wenyewe kama Wabunge kwa sababu hii mipango yote imekuwa ikipita mikononi mwetu hapa ndani ya Bunge na wote tumeitendea haki katika kuichangia

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko Kamati ya Bajeti, tumshukuru Mheshimiwa Waziri na Naibu wake na ofisi nzima kwa ushirikiano mzuri waliotupa na maelekezo na ndani ya mjadala ule yalikuwa ni mengi tumeyaongea, lakini kwa kweli naishukuru Wizara inafanya kazi nzuri na wako very responsive katika masuala yetu katika vikao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo machache tu ya kusema. Tukiangalia viashiria vya uchumi, kwa kweli ni hakuna namna zaidi tu ya kuwapongeza kwa sababu dalili za viashiria vya uchumi vyote viko vizuri na tunaenda vizuri. Ukuaji wa uchumi kulingana na malengo yetu ni kwamba ifikapo mwaka 2021 tunataka uchumi wetu ufike asilimia 10. Sasa hivi ni mwaka 2018/2019 tumefika 7%, tuna-gap ya 3% pale ambayo nahisi kwamba tunaenda vizuri, progress iko vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye mfumuko wa bei, bado tuko chini, sasa tumefikia asilimia 3.2 ambayo kwa kweli tunaona tunaenda vizuri. Hata hivyo, hapa ni lazima tuangalie, pamoja na kwamba tunaminya ule mfumuko wa chakula usiwe mkubwa ambapo unachangia kwa asilimia zaidi ya asilimia 28 sasa ni vizuri tuone, kwa sababu hapa inaonyesha kwamba kwa wawekezaji inawapa mileage nzuri kwa sababu they can plan. Vilevile kwa wazalishaji inaonyesha kwamba bei haibadiliki kwa kiasi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni vizuri wataalam waioanishe na riba tunazozipata kwenye mikopo. Kama inflation ya 3.2 siyo kubwa, vile vile na riba za kupata mikopo ili uweze ku-invest gharama zako na kupata faida, ni vizuri sasa pale wachumi muweze kutuchanganulia ili tuweze kuipata vizuri. Inaonekana kwamba huenda faida ya kuzalisha inakuwa ni ndogo kwa sababu mfumuko nao umebana sana, kama interest rate ya kwenye mabenki hujaibana vizuri. Kwa hiyo, hapo napo wataalam wetu wa mipango mtusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kwenye Sekta ya Kilimo, target yetu ni mwaka 2021 tunataka ukuaji uwe wa 7.6%. Sasa hivi tumefika 5.3%, tunakwenda, lakini Mheshimiwa Waziri wa Mipango tuangalie kwa kina ukuaji huu wa kilimo ambao unaajiri watu wengi hebu mkae mfanye retreat mwone ni wapi tunakosea? Kwa nini huu ukuaji usipande? Kwa sababu lengo letu tunataka tufike 7.6. Tutakapofika 7.6 kidogo mwananchi ataanza kuona pato kwenye mfuko wake. La sivyo, kama hatuwezi kwenda kwa namna hiyo na ku-invest na kutoa fedha kwenye vipaumbele vya Wizara hii, ukiangalia trend ya utoaji wa fedha kwenye za maendeleo kwenye kilimo saa nyingine hatufanyi vizuri, kwa hiyo lazima twende sasa tuweze kuwekeza pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bodi za mazao ambazo zinashughulika na kilimo cha wananchi wetu ni vizuri na ninashauri kwamba kwa kuwa sasa Serikali imeweka macho na Waziri Mkuu yuko huko kwa ajili mambo ya ushirika, tuongeze nguvu, tusipunguze nguvu ili wakulima wetu waweze kufaidi matunda yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija sasa kwenye mpango wenyewe ukiangalia mpango wetu kila kitu ambacho kinafanywa na Serikali ya CCM nchi hii, kiko kwenye mpango; lakini utakuta watu wanabeza au kuona kwamba hiki kitu ni kipya, hakikuwepo kwenye mpango. Mheshimiwa Waziri nakuomba, elimu ya mpango wowote tunaoutoa inaonekana haufiki kwa watu. Kitu kikija wanaona kwamba Serikali imekurupuka, hakikuweko kwenye mpango. Sasa ni vizuri bajeti ya kutoa elimu kwa ajili ya kuelimisha wananchi kwenye mpango, aidha Wizara yako, Kitengo chako kile cha Mpango ukipe bajeti kiwe kinaeleza mipango ya Serikali kwa kila sekta kwa miaka inayokuja ili wote tuweze kwenda pamoja. Inaonekana bado kuna information gap kati ya wananchi na mpango wenyewe.

Mimi bado najiuliza kitu kimoja, naipongeza Serikali, mnatoa fedha nyingi na zinaenda kwenye miradi, lakini utakuta mwenge wa uhuru ukipita kwa dakika tano kwenye mradi wanagundua kosa. Mwenge ukipita kwa dakika tano kwenye eneo lako, wanagundua kosa. Wizara walikuwa wapi? Wataalam walikuwa wapi? Mkuu wa Wilaya alikuwa wapi? Mkuu wa Mkoa alikuwa wapi? Waziri mhusika wa sekta alikuwa wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi vitu tunaweza tukaendelea kusema kwamba tuna fedha nyingi lakini kumbe miradi yote tunayoipelekea fedha inakuwa haina tija. Kwa hiyo, naomba kwa kweli tuangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulitunga Sheria ya Uhujumu Uchumi, sasa itoke kwa wafanyabiashara, iende sasa kwa wataalam. Wahujumu uchumi wawe ni wataalam ambao hawasimamii miradi vizuri. Fedha hizi zinakusanywa kwa wananchi kwa nguvu kubwa na tunatoa kodi kubwa, hii sheria sasa iingie maofisini, Waziri ajikute naye ameingia kwenye uhujumu uchumi, kwa sababu hakusimamia fedha alizozipeleka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hivyo, nirudi kwenye miradi hii ya kawaida. Mheshimiwa Waziri ulikopa fedha Euro milioni nane za maji katika mikoa ya Kigoma. Ubelgiji walitoa hizo fedha lakini miradi ile nayo haiendi. Sasa tukuulize na utuambie: Je, zile fedha zimeshatoka au imekuwaje? Maana yake miradi haiendi na hakuna kazi yoyote inayofanyika. Kwa hiyo, tunaomba kwa kweli uangalie hiyo miradi ya maji ambayo mmekopa fedha Euro milioni nane ili tuweze kwenda vizuri na miradi kote ilikopangwa iweze kutekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya PPP haitoshi Tanzania. Tunacho kitengo kizuri sana pale Wizara ya Fedha ambacho kinachushughulika na miradi ya PPP. Miradi ile tunaisoma kila wakati, hakuna kitu kinachofanyika. Tangu nimeingia Kamati ya Bajeti miradi ile inaletwa kwetu, tunaisoma, inachakatwa inafanyiwa nini, hakuna kinachoenda. Lazima PPP ifanye kazi iweze kuachia fedha za Serikali ili nazo zifanye kazi nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine, Mpango huu wa mwaka 2015 – 2021 tulisema unakuwa financed na shilingi trilioni 107. Tukasema watu binafsi watachangia shilingi trilioni 48. Tumeingia kwenye Kamati, Wizara haina data inayoonyesha private people wamechangia kiasi gani na hiyo miradi iko wapi? Sasa kama huwezi ku-track miradi iliyochangiwa na wawekezaji binafsi, lakini uliiweka kwenye mpango, hilo ni eneo ambalo lazima huo udhaifu tuweze kuuondoa. Tunataka kuona shilingi trilioni 48 za private sector imechangia wapi? Sehemu gani? Mradi gani? Kiwanda gani? Au project gani? Kwa hiyo, hiyo naomba kwa kweli tuweze kulii-improve vizuri ili tuweze kwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya umeme, barabara na afya, tunaomba speed ya ukopaji, kwa sababu wakati mwingine fedha ni za watu, kwa hiyo, tuongeze kasi ya kutafuta fedha hii miradi iweze kuendelea. Vijiji tunavyotajiwa ni vijiji ambavyo tunapeleka umeme, vinatugombanisha na wananchi kwamba umeme uko sehemu ya center, lakini kwenye vijiji ndani haujaingia. Kwa hiyo, ni vizuri tutafute fedha. Pamoja kwamba tumekopa mpaka tumefikia shilingi trilioni 53, tusiogope kwa sababu deni letu bado linahimilika, tuendelee kufanya hii miradi iweze kwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mpango sijaona mahali ambapo mafunzo kwa vijana yamesisitizwa sana. Vyuo vya VETA mna mpango wa kuvijenga, lakini kwenye mpango hakuna mahali ambapo pamesisitizwa sana. Naomba hapo kwenye Mpango tutakapourekebisha tuweze kuona mafunzo kwa vijana na ajira baadaye inakuwaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki kusema mengi, mengi tumeyaandika kwenye ripoti yetu ya Kamati, nafikiri inatosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.