Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nataka kwanza kusema kwamba siyo tatizo kuona fahari kuona fahari kwamba Rais wako anakuwa Mwenyekiti wa Jumuiya kubwa katika Kanda au popote pale. Hiyo siyo issue, kwa sababu ni rotationally. Vyovyote vile angekuwa mwingine yeyote angeweza kuwa Mwenyekiti kesho, kesho kutwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninachotaka kusema you should not politicize the issue, twende sober mind, tutazame nini tumshauri Mheshimiwa Rais wetu katika hicho kipindi anachokuwa Mwenyekiti, tutafanya nini kama Tanzania? Cha muhimu, tufanye ili legacy yake iwe na maana zaidi na siyo kumpongeza wakati baadaye hatafanya kitu cha maana, ili legacy yake ikumbukwe zaidi ya kuwa Mwenyekiti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, sisi ni member wa SADC, lakini katika mkutano ambao ni wa mwisho kabla Mheshimiwa Rais kuwa Mwenyekiti Serikali yetu imeshindwa kupeleka Wabunge kwenye Mkutano wa SADC uliokuwa Mozambique. Vile vile sisi tukiwa Wabunge wa SADC tumeshindwa katika mikutano mitatu kuhudhuria katika mikutano ya SADC. Picha hii haiwezi kuwa nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi tuna mkutano hapa kwetu, lakini kuna utamaduni wa SADC wa kukaribisha NGOs, tunaambiwa kwamba wana-NGOs wengi walikuwa harassed walipokuwa Dar es Salaam; wakasachiwa wakapekuliwa wakafanyiwa kila kitu. Sisi kama SADC tuna itifaki ya kufanya election observations, lakini katika mikutano uchaguzi kibao hatuendi, tunacha legacy gani kama Taifa? Kuna Model Laws na visions za SADC ambazo zinataka nchi zifanane kwa kadri inavyowezekana. Kama nchi hatufanyi vizuri katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi SADC inajengwa kuwa Bunge kamili baadaye. Tungeomba Rais wetu asaidie watakaokuja baadaye katika Bunge lingine walikute Bunge la SADC limekaa sawa sawa, role yake iwe nzuri hiyo.

Mheshimiwa Spika, cha pili, nakuja kwenye uwekezaji. SADC ina watu karibu 370 wengine wanasema 350 jumla yake, wana GDP ya milioni 6.07 kwa pamoja, lakini pia SADC inasemekana kwamba ina-perform low by 25 percent ya uwezo wake, kwa maana bado biashara miongoni mwetu iko ndogo sana. Kwa mfano, Tanzania tunafanya vizuri na South Africa pengine na Democratic Republic of Congo, lakini sisi kama Taifa hatufanyi vizuri na nchi nyingine. … Katika hili tulifanye vizuri.

Mheshimiwa Spika, pia kama zone hii kuna tatizo kubwa la zone phobia South Africa. Hii inafanya kusiwe na uzuri wa nchi nyingine kushiriki baina yao pamoja. Tungemshauri Rais wetu hili alisimamie vizuri ili zone phobia na kufungua mipaka kuwe kuzuri na kwa Mataifa yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, pamoja na kusema kwamba tumefurahi kwamba Rais wetu amekuwa Mwenyekiti wa SADC, ni mwaka mmoja tu, lakini muhimu legacy gani ataacha ili tuje tufurahi kama Watanzania ametufanyia chema kwa ajili ya nchi yetu?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana Mheshimiwa Spika.