Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze mchango wangu kwa kumshukuru Mungu kwa kuniamsha salama na kuendelea kunijalia uhai na kunipa uwezo wa kujadili hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze mchango wangu kwanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu wa Wizara hii pamoja na wakuu wote wa majeshi yetu yote. Kwa kweli, kazi inayofanywa na majeshi wanastahili pongezi na heshima iliyotukuka kwa kuilinda nchi yetu ndani na nje ya mipaka yetu. Askari wetu wanafanya kazi kwa weledi mkubwa, nasema hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuacha kuwaingiza kwenye mfumo wa Bima ya Afya (NHIF) askari wetu sio jambo jema. Familia za askari wetu zinahangaika sana na masuala ya afya kwani hakuna hospitali bora kwenye vikosi/makambi ya majeshi yetu na zipo pia familia zinazokaa uraiani mbali na Kambi za Jeshi, hivyo wanapopata uhitaji wa matibabu wanapata shida sana. Serikali ione umuhimu wa kuwaingiza askari wetu kwenye utaratibu wa bima ya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko pia tatizo la malipo ya posho za maaskari wetu. Wako maaskari wengi wanaodai posho mbalimbali kama vile posho za likizo, posho za madaraka na mengine kama hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la pili kwa majeshi yetu ni muda wa kuingia na kutoka kazini. Ili askari awahi kuingia kazini inamlazimu kutoka nyumbani saa 11:00 alfajiri au saa 10:30 na jioni wakitoka saa 11:00 wanafika nyumbani zaidi ya saa 03:00 usiku. Hawa ni wale wanaokaa nje ya makambi ya majeshi yetu, hivyo kuwafanya askari wetu kukosa utulivu wa kikazi maana muda mwingi wanashinda kwenye daladala, hasa kwa askari wanaoishi Dar es Salaam.