Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo kadhaa nataka majibu ya Serikali. Majeshi yetu kupelekwa Darfur na Congo DRC, kwa nini mpaka leo majeshi yetu yanapelekwa Darfur na Congo DRC? Malipo yake kwa Taifa hili kwa sasa ni shilingi ngapi? Fedha za malipo zinachangia bajeti kiasi gani? Ukombozi wa Afrika umekwisha, Watanzania wengi wameuawa sana, hakuna malipo kutoka kwa nchi tulizokomboa mfano South Africa, Namibia, Zimbabwe, Mozambique na nyingine nyingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeanza kupeleka Watanzania wengi kuuawa bila malipo kwa muda mrefu, sasa hivi imefika wakati wa nchi kuomba malipo kwanza kabla ya kupeleka vijana wetu kuuawa, Congo kwa mfano kuna madini mengi na wanajeshi wetu wanauawa huko kila siku. Naomba watulipe fedha au madini ili tujenge uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani sasa hivi hakuna nchi inapeleka watu wake vitani nchi nyingine bila malipo makubwa. Serikali ituambie wale wanajeshi waliouawa mwaka jana na mwaka juzi Congo DRC fidia imelipwa kiasi gani? Leo kuna wanajeshi wanapelekwa Darfur miaka mitatu wakati Omar Al-Bashir amefukuzwa, hakuna amani, nani anatulipa? Umoja wa Mataifa inalipa kiasi gani kwa thamani ya watu wetu wanaenda kuuawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka tulienda kumuondoa Mohamed Bakar kule Comoro kwa maslahi ya Wacomoro tulilipwa bei gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Rwanda tunaisifia kuwa iko juu kiuchumi na kwamba Kagame anajenga uchumi wake. Kazi yake amepeleka majeshi Congo DRC anachochea vita, wanateka maeneo ya madini, wanachimba na kuuza then wanajenga uchumi wa Rwanda. Sisi Jeshi letu tunapeleka kuuawa bure bure tu, haikubaliki.