Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie kidogo kwenye Wizara hii nyeti, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu sana kati ya Jeshi la Wananchi Mikumi na wananchi wa Kitongoji cha Vikweme. Nilishalifikisha jambo hili kwa Mheshimiwa Waziri na nilishauliza swali hili mara kadhaa hapa Bungeni bila mafanikio, Mji Mdogo wa Mikumi wapo tayari kabisa na wameshatenga eneo kwa ajili ya kuwapa Jeshi ili wakafanyie huko mazoezi, lakini Jeshi letu limekataa na kuendelea kuling’ang’ania eneo la Vikweme ambalo wananchi wengi wa Jimbo la Mikumi wanalitegemea kwa kilimo na pia kuna nyumba za wananchi kwa makazi, shule, nyumba za ibada na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba sana Waziri aweze kulitatua hili na pia afanye ziara jimboni Mikumi kama alivyoniahidi wakati akijibu swali langu Bungeni.