Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Bajeti ya Wizara; ninapenda kuishauri Serikali kuongeza bajeti ya Wizara hii kwani imeshindwa kufanya shughuli zake kwa ufanisi. Mfano, Mkoani Pwani, Wilaya ya Kibaha kuna Kambi ya Nyumbu na Msangani. Matatizo ya Msangani na Nyumbu ni tangu enzi za awamu ya kwanza za mwasisi wa Taifa hili, ndiyo barabara inayoelekea kwenye kambi hizo ilitengenezwa, ni mbovu na ni shida kiasi hata wanaofanya au watoa huduma katika majeshi hayo hupata shida kufika huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Jeshi la Nyumbu; enzi za Mwalimu, Nyumbu iliweza kutengeneza mpaka gari kwani Nyumbu ina mashine na mitambo ambayo iliwezesha kufanya kazi kwa ufanisi lakini leo hii Nyumbu tuliyoitarajia kuleta mapinduzi ya viwanda majeshini imepotea. Hali hii imesababisha wananchi na vijana waliokuwa wamepata vibarua kukosa ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la migogoro ya mipaka na raia; nitoe ushauri Serikalini kuhakikisha inafuatilia mipaka hiyo na maeneo yote ya Jeshi yapimwe na kupata haki za umiliki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira Jeshini ni tatizo, kuna vijana walioahidiwa kuajiriwa baada ya kujenga Mererani na pia wapo wa Operesheni Kikwete waliahidiwa kuajiriwa lakini mpaka sasa wapo mitaani na tunajua wanajua matumizi ya silaha, hivyo kuwaacha mtaani ni hatari. Operesheni Magufuli nao wapo mtaani, je, hii si hatari kubaki na vijana bila kupewa shughuli za kufanya?