Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. MUHAMED AMOUR MUHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote ni vyema tukamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kunipa uhai na uzima na kuniwezesha kuchangia mada iliyopo mezani ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Nianze kwa kuzungumzia mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia kuhusu maeneo yaliyochukuliwa na JWTZ kutoka mikononi mwa wananchi; kwa miaka mingi sasa baadhi ya maeneo hayo wananchi hawajafidiwa, kwa mfano kule Zanzibar sehemu inayoitwa Kiongwe Jeshi limechukua eneo ambalo wananchi walikuwa wakilima na kufugia wanyama wao, lakini pia hili eneo ni mali yao. Kwa miaka mingi tunavyozungumza wananchi hawajapata fedha zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Serikali iwaonee huruma wananchi hawa kukatwa fedha katika mafao yao baada ya kustaafu. Kupitia awamu hii askari wastaafu wamekuwa wakikatwa asilimia 20, hii ni hatari, niiombe Serikali ifikirie tena hali ya kuwabakishia wastaafu hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kitengo cha Bahari, hapa napo pana mazonge makubwa, JWTZ linatumia force kubwa sana ya kutisha kupambana na wavuvi wetu ambao pia ni raia wa nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, suala la license haieleweki dhahiri hasa ni license ya aina gani inayotakiwa na hapa wavuvi kutoka Zanzibar wamekuwa wakisumbuliwa kwa aina ya license inayohitajika. Aidha, baadhi ya nyakati hupigwa na kuumizwa vibaya. Niiombe Serikali iliangalie hili kwa huruma sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.