Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, ubia wa SUMA JKT na Holley wa kununua hisa za milioni 744 mwaka 2007 na kutengeneza Tanzansino kwa lengo la kuzalisha dawa na bidhaa za madawa. Wabia hawa hawakuelewana, mkataba ukavunjika na kugawana mali na sehemu ya ardhi ya Jeshi ilikuwa sehemu ya mkataba. SUMA JKT wakalazimika kulipa fidia ya fedha kunusuru eneo la Jeshi kuwaangukia mkononi. Swali, ipi ilikuwa nia ya SUMA JKT kuingia ubia wa biashara ya namna hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba wa SUMA JKT na CAMI ukiitwa CAMISUMA ukiwa na lengo la kuzalisha nguo na kusambaza (CAMISUMA Garments) 2006; SUMA 39% na CAMI 61%. Jeshi lililipa milioni 10 kwa ajili ya umeme na huduma mbalimbali kwenye hivyo viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, SUMA JKT na Equator Automatic Co. Ltd; SUMA 30% na Equator 70%. Kuunganisha magari makubwa, basi, mashine za kilimo, magari ya zimamoto etc., mkataba umevunjika na mchakato wa ku-windup unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, SUMA JKT na Chenggong Ltd.; Tanzania 80% na Chenggong Ltd. 20%. Lengo ni kukodisha, kuuza vifaa na mitambo mikubwa ya ujenzi, bulldozer, caterpillar etc. Mkataba uliingiwa mwaka 2015 ila upembuzi yakinifu ulifanyika 2016.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkataba wa matrekta ya SUMA JKT (2015) na Kampuni ya Ursus SA kutoka Poland wenye thamani ya bilioni 119.9; lengo kuuza matrekta na vipuri vyake na huduma nyinginezo. Mkataba huu pia haukukamilika, swali, kuna shida gani JKT?

Mheshimiwa Mwenyekiti, manunuzi mbalimbali yamefanyika bila kufuata taratibu au bila kupitishwa na bodi. Manunuzi yenye thamani ya 1,114,565,015 kwa mujibu wa report ya CAG 2015/2016 katika Fungu 39.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajeshi kupewa bima ya afya; hiki kiwe kipaumbele kwa kuwa huduma ya matibabu kwenye hospitali ya jeshi haijasambaa nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umri wa miaka mitatu hadi sita kabla ya mwanajeshi kuoa ni mrefu mno kiasi cha kupelekea vijana hawa kujiingiza katika uasherati au wanawake kuchelewa sana kupata watoto ukizingatia kuwa umri wa kuzaa huwa unapita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupanda vyeo/ madaraja na mshahara; Jeshi liendelee kuhimiza uzalendo huku Serikali ikitimiza wajibu wake wa nyongeza ya mishahara na madaraja.