Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kuhusu mipaka, Jeshi limekuwa linapiga na kuvunja na kubomoa nyumba za wananchi, kuchukua sheria mkononi kwa Jeshi siyo kitu sahihi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia za wananchi kwa maeneo yao ina suasua kabisa na ikibidi kama ikishindikana warudishiwe maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu viwanda Jeshini, kuingia uchumi wa viwanda ni vyema tukawekeza katika viwanda vilivyoanza vya Jeshini kwani ni nguvu kazi iliyo tayari na ya uhakika lakini ukosefu wa fedha na kuwarudisha nyuma vifaa chakavu vinakwamisha ufanisi wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa mipaka, Jeshi lipatiwe vifaa na pesa zaidi ili kuhakikisha mipaka yetu inakuwa salama kama uwepo wa boti za doria na helkopta za ulinzi, ujenzi wa madaraja ya kupitisha vifaa vizito nyakati za dharura ni muhimu sana.