Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ZAINAB M. AMIR: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Mbunge na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa kazi nzuri anayoifanya katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali bajeti itakayopitishwa na Bunge itolewe kwa wakati ili kuweza kusaidia Wizara kutekeleza miradi ya maendeleo iliyokusudiwa kutekelezwa. Serikali imshauri Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano pindi anapofanya uteuzi wa Maafisa wa Jeshi katika ngazi mbalimbali, angalau azingatie jinsia, maana takribani maafisa wa juu wote wa Jeshi ni wa jinsia ya kiume, takribani 90%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ione umuhimu wa kuwapatia bima ya afya wanajeshi wetu wote hapa nchini pamoja na familia zao kuliko kutegemea kupata matibabu katika hospitali za kijeshi maana wakati mwingine wanajeshi hawa hulazimika kutumia gharama (fedha zao) kugharamia matibabu katika hospitali ambazo siyo za Jeshi. Hivyo bima ya afya ni muhimu kwa wanajeshi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kwa wale wanajeshi ambao wamepata mafunzo au kozi ambayo itawawezesha kupandishwa vyeo kutokana na mafunzo hayo, wapewe haki yao ya kupandishwa vyeo hivyo. Serikali iwajengee nyumba za kutosha Maafisa wa Jeshi, pia wanajeshi wetu ili wawe na makazi bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iweke mipaka upya katika maeneo yote ya Jeshi nchini ili kuondoa migogoro ambayo inaendelea baina ya Jeshi na wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho namuomba Mwenyezi Mungu azidi kumpa afya njema na umri mrefu Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Mbunge na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili aweze kuendelea kutekeleza majukumu yake yote katika Wizara hii.