Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Zainabu Mussa Bakar

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ZAINAB MUSSA BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni muhimu sana hasa ukizingatia ni Wizara ya Ulinzi wa nchi, mipaka yetu na kulijenga Taifa letu liwe bora na salama. Serikali ione umuhimu ya kutoa fedha zilizoidhinishwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya kuboresha mfumo wa mawasiliano salama Jeshini chini ya Fungu 57. Hii ni muhimu sana kwa utekelezaji wa mfumo wa mawasiliano ambao utasaidia katika kutekeleza majukumu yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali itoe fedha zote zilizoidhinishwa kwa ajili ya utunzaji wa zana, magari na mitambo katika mwaka wa fedha 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunaitaka Serikali kulipa madeni ya kimkataba kwa kutenga fedha zaidi kwenye miradi ya maendeleo Fungu 57. Tunaitaka Serikali kutoa nyongeza ya mishahara kwa wanajeshi wetu. Kwani hili ni hitaji la kisheria na kikanuni na pia ni kichocheo cha ari ya kufanya kazi kwa bidii zaidi. Serikali itoe kipaumbele kwa maslahi ya wanajeshi kwa kuwa ni kada ambayo imejitoa kwa gharama ya uhai wao katika kulinda mipaka ya nchi yetu dhidi ya adui yoyote kutoka nje na kuhakikisha kwamba lipo salama wakati wote. Kwa hiyo, si vizuri wanajeshi kuanza kulalamika kwa suala hili ambalo ni stahiki yao ya kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali isifanye suala la kisiasa ama ubabaishaji katika kuwapandisha vyeo wanajeshi. Tunaitaka Serikali iwapandishe vyeo wanajeshi wote wanaostahiki kulingana na sheria, sio nusu wapandishwe na nusu hawapandishwi, huo si uadilifu. Kuna malalamiko kwamba wanajeshi 8,000 waliofuzu kupandishwa vyeo mwezi Desemba, 2018; lakini ni 4,000 tu waliopandishwa na ilhali sifa wanazo. Je, Serikali ituambie ni lini watawapandisha vyeo wanajeshi hao?