Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. LUCIA U. M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za maendeleo zimekwenda asilimia ndogo sana, asilimia 18 tu hadi sasa na kipindi kilichobaki ni mwezi mmoja tu kuisha mwaka wa Serikali. Naitaka Serikali ipeleke bajeti iliyosalia kipindi hili kilichobakia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maslahi ya wanajeshi na polisi; kwa kuwa kazi hii ya uanajeshi au polisi ni kazi hatarishi inahitaji motosha, naomba Serikali ihakikishe inawapa motisha na kuongeza maslahi ya wanajeshi na polisi. Mavazi ya wanajeshi yatolewe pale wanapohitaji maana kazi yao inahitaji mavazi kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bima ya wanajeshi, wanajeshi hawana bima za afya, naitaka Serikali iwapatie bima za afya wanajeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kauli za vitisho, kumekuwa na kauli za vitisho kwa wananchi. Wananchi wengi sasa hivi wamejengwa na woga badala ya Jeshi kuwa kimbilio. Naomba Wakuu wa Majeshi wawe na kauli zinazohamasisha utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.