Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali juu ya mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara ni ndogo jambo linalosababisha mazingira magumu ya utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuishauri Serikali juu ya Mradi wa Bagamoyo Special Economic Zone. Mradi huu umeingiza hasara kwa kutokutekelezwa mpaka sasa. Tukumbuke kuwa fidia kubwa imelipwa ikiwa ni fedha za walipa kodi na ni muda mrefu. Je, hiyo fedha ingeingizwa kwenye mradi mwingine, tungekuwa wapi sasa hivi? Fedha nyingi zimetumika kwenye kuhakikisha kuwa mradi huu unalitoa Taifa letu hapa lilipo kuelekea uchumi wa kati kwa kuifanya reli kupokea mzigo mkubwa toka bandarini kubeba na reli zetu kuelekea kwenye nchi nyingi zisizo na bandari.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Bagamoyo na Mkoa wa Pwani walitoa maeneo yao wakijua kuwa nao vipato vyao vitaongezeka kwa bandari hiyo kujengwa, kwani wangepata ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, tozo za TFDA zinatozwa kwa fedha za kigeni na kwa kila product inayotengenezwa nembo yake na kwa gharama kubwa. Hivyo, tunawavunja moyo wajasiriamali wadogo ambao ndio kwanza wanajikusanya kwa mitaji midogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni TRA. Naomba kuishauri Serikali kuacha kutoza kodi on capital basis kwani unamkadiriaje mteja anayeanzisha biashara wakati hajaanza biashara? Hii imefanya watu wengi kushindwa kuendeleza biashara zao, kwani mitaji yao inakuwa imemezwa kwenye kodi kabla ya biashara kuanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni ufungaji biashara. TRA badala ya kujadili na wafanyabiashara ndipo wafunge au wapewe muda wa kulipa kidogo kidogo wanafunga biashara. Hii ni kuipa hasara Serikali.