Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Wizara hii. Mheshimiwa Kakunda Waziri wa viwanda na Biashara na Naibu wake Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu utahusu maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni tozo ya usafirishaji kwa wafanyabishara. Kuna malalamiko ya wafanyabiashara kuwa na tozo nyingi na taasisi nyingi za udhibiti. SUMATRA, Zimamoto, TFDA, OSHA, TRA, Mamlaka ya Serikali za Mitaa, WCF na zinazofanana na hizo. Tozo zifuatazo; Corporate Tax, Service Levy, OSHA, TFDA, TBS, tozo ya ukaguzi wa Zimamoto, nashauri kuwe na kituo kimoja cha ulipaji tozo hizo na taasisi zipunguzwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri viwanda vya korosho vilivyobinafsishwa vifufufuliwe na vifanye kazi ya kubangua korosho. Wanunuzi wengine wanafanya maghala, nashauri wanyang’anywe. Tuwe na mkakati mahsusi wa muda mfupi wa kuuza nje korosho zilizobanguliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, SIDO ni taasisi ambayo inaweza kuwakomboa wakulima na wajasiriamali wengine katika kutoa teknolojia mpya katika uzalishaji. Naomba taasisi hii ipewe fedha za kutosha ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi. Pia maonyesho ya SIDO yaboreshwe na teknolojia zinazotumika ziwe za kisasa. Aidha, kuwe na utaratibu wa kuwasilisha teknojia hiyo kwa wakulima au wajasiriamali wa vijijini.