Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Naibu Spika, nasimama kwa heshima na unyenyekevu mkubwa, kwanza kabisa kuipongeza Wizara husika kwa juhudi zao katika kuinua Tanzania ya viwanda na hata kueneza falsafa ya Tanzania ya Viwanda. Hili ni jambo ambalo mimi binafsi naona ni vyema kupongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujikita kwenye maeneo mawili. Mosi, utekelezaji wa mradi wa makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma, pamoja na ushiriki wa vijana kwenye uchumi wa viwanda na biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapofanya mapitio ya report ya Wizara, page ya 15 sura ya 28, 29 na 30, nadiriki kusema Wizara ya Viwanda na Biashara pengine iridhie kuendesha sehemu ya sentensi inayosomeka kwenye sura namba 29 ambayo kwangu naona ni upotoshaji mkubwa kwa Taifa, hasa tunapofanya marejeo ya Ilani ya Chama Tawala sambamba na utungwaji wa sheria mbili za ulinzi wa maliasili za nchi (Natural wealth Resources Permanent Sovereignty Act, 2017) pamoja na Sheria ya Natural Wealth and Resources Contract Review Renegotiation of Unconscionable Terms 2017).

Mheshimiwa Naibu Spika, ninasema ama naishauri Wizara kufuta kipengele hiki chote kwa sababu moja; sababu za mkandarasi kuomba vivutio vya ziada hauna nafasi kwenye sheria zote mbili, kwa sababu sheria hizi mbili au hususan Sheria inayohusu mapitio ya mikataba yenye masharti hasi, hakuna mahali popote inapo-deal na maombi ambayo yako nje ya mkataba. Ikumbukwe na kama ilivyoandikwa na Wizara ukurasa wa 15, ombi la mwekezaji la kuomba vivutio vya ziada havikuwepo kwenye terms za mkataba, kwani hii ni addition incentives na siyo sehemu ya mkataba.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara inapotosha kwa kueleza Umma na Watanzania kwamba mkataba wa Liganga na Mchuchuma umekwama kwa sababu moja ya matakwa ya sheria zote hizi mbili; ni pamoja na kufanya mapitio ya mkataba kati ya NDC na Sichuan Hangda Group na kwamba baada ya Mkandarasi kutaka vivutio vya ziada hii imesababisha Wizara kufanya mapitio ya mkataba. Huu ni uwongo kwa sababu tunapofanya Part III inayoeleza procedure on how to deal with the Review Renegotiation of Unconscionable Terms, imeweka bayana utaratibu wa kisheria utakaotumika kufanya mapitio haya ya mikataba yote iliyoonekana kuwa na masharti hasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, najiuliza, inakuwaje leo Wizara inatuambia kutokana na masharti hasi ya mkataba wa Liganga na Mchuchuma, basi mchakato wa kufanya mapitio unaendelea na angali jukumu hilo ni la Bunge? Naishauri Wizara irejee sheria ya masharti hasi Ibara ya 4(1) – (5), inasema bayana kwamba jukumu la kufanya mapitio ya mikataba hasi ni la Bunge. Rejea pia Katiba ya Nchi Ibara 63(2), hii ni kwa kuwa mradi wa Liganga na Mchuchuma hauna unyeti wowote (sensitivity) kama ambayo ingekuwa ni mradi wa chini ya Taasisi ya Idara za Usalama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wizara husika imetuambia kuwa mchakato wa mapitio ya mkataba wa Liganga na Mchuchuma unaendelea: Je, ni lini Bunge lako Tukufu liliwahi kutoa azimio la mapitio ya mkataba wa Liganga na Mchuchuma? Kwani ukirejea mkataba wa masharti hasi, ni lazima Bunge lako litoe azimio la kufanya mapitio ya Liganga na Mchuchuma, kitu ambacho hakikuwahi kutokea. Sasa ni kwa nini tunaambiwa mchakato unaendelea? Rejea Part II 5(3) of this Act.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaongelea umuhimu wa kuendelezwa kwa mradi wa Liganga na Mchuchuma kwa sababu vijana wetu hawana ajira na pia ukiangalia pamoja na chuma kinachozalishwa nchini, Tanzania ni asilimia 80 na asilimia 20 tu ndiyo inayoagizwa nje ya nchi, lakini bado ajira hailindwi. Kati ya ajira 23,150,000, ajira 20,000,000 zote ni ajira za muda ambapo ajira za muda mrefu ni 3,150 tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye mchango wangu wa ushiriki wa vijana kwenye Sekta ya Biashara na Viwanda, ikumbukwe Bunge lako hili Tukufu lilipitisha kusudio la kushirikisha vijana kwenye zabuni (tenders) ambapo vijana walionekana wenye kuwapa nafasi/dirisha maalum ili waweze kushiriki rasmi kwenye michakato ya zabuni, lakini swali langu kwa Wizara: Je, ni kwa nini kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri hakuna taarifa yoyote inayohusu ushiriki wa vijana kwenye Sekta ya Viwanda na Biashara?

Mheshimiwa Naibu Spika, nchini Kenya upo mfuko maalum Youth Enterprises Development Fund ambapo vijana wenye umri kati ya miaka 18 - 35 walihusishwa kikamilifu. Haitoshi, pia nchi ya Kenya imekuwa ikitenga kiasi cha fedha kwenye kila Bajeti yao ya mwaka wa fedha ambapo five years back mfuko huu ulikuwa na USD 940,000. Malengo ya mfuko huu ni pamoja na kutoa startup capital, create Mark space and incubators for young graduates and dropout students.

Mheshimiwa Naibu Spika, halikadhalika nchi yetu ya Tanzania chini ya Wizara hii imekuwa na Mfuko wa Maendeleo ya Wajasiliamali Wachanga (NEDF) ambapo last financial year ilitengwa shilingi bilioni 15 ambayo haikuwahi kutoka hata senti moja. Ushauri wangu kwa Serikali, iweze kutoa fedha angalau asilimia 50 ya fedha ya maendeleo. Last financial years kati ya shilingi bilioni 100 ilitoka shilingi bilioni 12, fedha za maendeleo. Serikali ikiweza kutoa at least asilimia 50 ya fedha za maendeleo, basi Mfuko wa NEDF uongezewe fedha hata kufika shilingi bilion 50 - 100 ili vijana wengi zaidi waweze kupata start up capital na hata suala la uhaba wa ajira uondoke.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.