Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu, nashukuru sana nami nichangie katika Wizara hii muhimu ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, COSOTA; kwanza kabisa ningependa kuishauri Serikali ihamishe COSOTA kutoka kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara na kuipeleka kwenye Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Hii itasaidia sana kuifanya kuwa kwenye Wizara inayohusiana kabisa na masuala yao ya sanaa ambayo ni Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, changamoto inayowakabili wasanii wa nchi hii ni wizi wa kazi za wasanii na sheria inayolinda kazi za wasanii Sheria Na.7 ya mwaka 1999 imepitwa na wakati na kwa kweli imekosa meno kabisa na imeshindwa kabisa kuwalinda na kuwasaidia wasanii wa Tanzania ambao kila kukicha kazi zao zinaibwa na kuuzwa kiholela na hakuna sheria inayowabana wezi wa kazi za wasanii. Naiomba sana Serikali kama kweli inataka kuwasaidia wasanii wa Tanzania basi iilete hapa Bungeni Sheria ya Hati Miliki na Haki Shiriki Na.7 ya mwaka 1999 tuifanyie marekebisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vidogo vidogo vya kuchakata mazao ya kilimo na vya kuchakata mazao ya mifugo; Jimbo la Mikumi linalima sana mazao mbalimbali, lakini tuna tatizo kubwa sana la viwanda vidogo vidogo vya kuchakata mazao hayo ambayo yangeweza sana kutoa nafasi kwa wananchi wa Mikumi kuweza kupandisha thamani ya mazao yao kwa kuyachakata kwenye viwanda hivyo. Naiomba sana Serikali iweze kulitilia mkazo hili ili tuweze kuwasaidia wakulima wetu ambao wanalima kwa bidii zote, lakini masoko yamekuwa ni kitendawili kikubwa sana kwao, hasa kwenye Kata za Tindiga, Kilangali, Kisanga, Uleling’ombe, Mhenda, Ulaya, Masanze, Zombo, Vidunda, Ruhembe, Mikumi, Kidodi, Mabwerebwere na Kata ya Malolo. Hivyo tunaomba sana Serikali iangalie suala hili muhimu kwa kutusaidia tupate viwanda vidogo vya kuchakata mazao ya kilimo na viwanda vya mazao ya mifugo kama viwanda vya nyama, ngozi, maziwa na kadhalika ili tuweze kuwasaidia wakulima na wafugaji wa Jimbo la Mikumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.