Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata fursa ya kuchangia Hotuba ya Wizara hii ya Viwanda na Biashara. Napongeza hotuba hii na naomba kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tuna dhamira ya kweli ya kujenga uchumi wa viwanda na biashara, ni lazima tuoneshe kwa vitendo. Kwa kuanzia na mkakati wa makusudi wa kutenga bajeti kubwa na ya kutosha kukidhi mahitaji ya kujenga mazingira yote wezeshi ya uwekezaji kwenye viwanda na biashara. Bajeti inayotengwa ni ndogo na inayotolewa ni ndogo zaidi, 30% kwenye matumizi ya kawaida na 6% maendeleo, ni ndogo mno kwa sekta muhimu kama hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji bado hii ni changamoto kubwa. Mwaka 2010 Serikali iliunda task force ya kutengeneza roadmap ya kuboresha mazingira ya uwekezaji baada ya kupata rank mbaya toka survey za kimataifa. Kwa hiyo Wizara nane kama Fedha, Viwanda, Kilimo, Uwekezaji, Nishati, Miundombinu, Ardhi na Maji wakapitisha roadmap iliyozingatia mambo yafuatayo:-

(i) Kurahisisha utoaji wa vibali vya ujenzi;

(ii) Ukaguzi wa maeneo ya biashara;

(iii) Ku-streamline malipo ya kodi mara mbilimbili kupitia taasisi mbalimbali;

(iv) Kuweka wathamini wa Serikali wa kikanda; na

(v) Kupitia sheria zinazoruhusu mlolongo wa roadblocks.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hii taskforce, Ofisi ya Waziri Mkuu iliratibu pamoja na wadau utayarishwaji wa mpango wa utekelezaji. Uliendelea na utekelezwaji wa maeneo yenye quick wins, kutengeneza mpango wa ufuatiliaji na tathmini na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, hiyo roadmap imefikia wapi katika kuboresha mazingira ya biashara? Sasa mwaka uliopita tukaja na blue print na yenyewe inatokana na ranking yetu kwenye doing business imeshuka, sasa vimefikia wapi? Win wins ziko wapi, mbona hali imezidi kuwa mbaya?

Mheshimiwa Naibu Spika, Kurasini Logistics Park, huko nyuma ililenga kutumia eneo ambalo lingekuwa kitovu cha biashara kati ya China, Tanzania na nchi zote za jirani yetu hadi Afrika ya Kati, chini ya ubia wa Tanzania (EPZA) na kampuni ya China. Tanzania ilikuwa kati ya nchi nne Afrika zilizoteuliwa kufaidika na uwekezaji huo na kuboresha biashara kati ya China na Tanzania. Sasa kwa nini tunabadilisha matumizi na kuingiza suala la kuunganisha magari?

Mheshimiwa Naibu Spika, majadiliano na maamuzi yanachukua muda mrefu sana, hii inakatisha tamaa wawekezaji na kuongeza gharama na kujenga mazingira ya rushwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, miundombinu inayoenda kwenye viwanda vingi nchini na hata katika maeneo ambayo yamelengwa uwekezaji mkubwa mfano Mradi wa Liganga, Engaruka, viwanda vya Coca-Cola, TBL, Mbeya, Kilimanjaro na viwanda vingi vya Dar es Salaam, Chang’ombe na Keko.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.