Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote kwa kuleta hotuba nzuri. Nampongeza pia Mwenyekiti mpya wa Bodi ya TANTRADE aliyechukua nafasi niliyoiacha wazi baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Buyungu. Kipekee nampongeza Director General wa TANTRADE, Ndugu Edwin Rutagezuka kwa utendaji wake mzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya pongezi hizo nipende kuchangia na kushauri katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi ya vitambulisho vya Taifa katika kurasimisha biashara; kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, hadi sasa, vitambulisho vya NIDA vilivyopatikana ni takribani milioni 16 tu katika nchi nzima. Sharti la kutumia vitambulisho hivyo katika kurasimisha biashara lililowekwa na BRELA limezuia malalamiko kutoka wajasiriamali wengi ambao wanashindwa kusajiri na kurasimisha biashara zao kwa kutokuwa na vitambulisho hivyo. Ushauri wangu ni kwamba, BRELA iendelee kutumia vitambulisho mbadala hadi hapo Serikali itakapokuwa imewapa Watanzania wote vitambulisho vya Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, utafutaji wa masoko ya mazao ya kilimo; masoko ya mazao ya kilimobado ni changaoto kubwa ukizingatia kwamba bei za mazao zinatawaliwa na uzalishaji katika nchi zinazotuzunguka na mahitaji yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri TANTRADE ijikite katika kufuatilia ubora wa mazao ya kilimo kwa matumizi ya chakula na viwanda kutafuta masoko ya mazao ya chakula, ni vema TANTRADE ishirikiane na Mashirika ya Kilimo na Chakula ya Kimataifa kama FAO na WFP ili kuwa na takwimu halisi za mahitaji ya mazao na kuwaelekeza wafanyabiashara kutafuta masoko hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, ni muhimu TANTRADE ishirikiane na Wizara nyingine kama vile Wizara za Mambo ya Nje na Kilimo ili kubaini vikwazo vya usafirishaji wa bidhaa (mazao) kutoka Tanzania kwenda katika nchi nyingine ili kuviondoa. Mifano iliyopo ni pamoja na vikwazo vya kusafirisha mazao ya chakula kwenda katika nchi za Sudan Kusini kupita Uganda, Kenya, Burundi, Rwanda na Congo DRC. Kipekee napenda kujua status ya soko la muhogo la China.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuanzisha vituo vya kuunganisha zana za kilimo. Inakadiriwa kuwa Tanzania ina eneo la hekta milioni 44 zinazofaa kwa kilimo ambapo eneo linalolimwa hadi sasa ni kama hekta milioni 10.1 tu (I stand to be corrected). Hata hivyo, eneo linalolimwa kwa kutumia zana (very roughly) ni kama ifuatavyo:-

Eneo linalolimwa kwa jembe la mkono 70%, eneo linalolimwa na wanyamakazi 20% na eneo linalolimwa kwa matrekta 10%, jumla 100%

Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri, kwa kuwa ni vigumu kwa kila mkulima kumiliki trekta, ni vema Serikali ianzishe vituo vya kuunganisha, kukodisha na kuhudumia (serving) vituo vya zana za kilimo, yaani Tractor Assembling, Hiring and Service Centers) ambavyo vinatoa huduma kwa wakulima wetu ili walime maeneo makubwa zaidi. Vituo hivyo vitasaidia pia kutoa ajira za mafundi mbalimbali watakaoandaliwa na vyuo vya ufundi.

Mheshimiwa Naibu Spika, uanzishaji wa Saturday Bonanza; wakati nikiwa Mwenyekiti wa TANTRADE, tulikuwa na mawazo ya kuanzisha magulio wa ajili ya kuwaelimisha wafanyabiashara wasio rasmi (Almaarufu-Machinga) ili waweze kutumia viwanja vya maonesho (SABASABA- Mwalimu Nyerere) Dar es Salaam. Je, mchakato huo umefikia wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kwa kutumia mfumo huo, tungeweza kuwasaidia Wamachinga na kujua wenye bidhaa wanazoziuza na kuiwezesha Serikali kupata ushuru unaostahili kuliko hali ilivyo sasa mitaani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.