Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Zainab Mndolwa Amir

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. ZAINAB M. AMIRI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nitoe shukrani kwa Wizara ya Viwanda na Biashara, nampongeza Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara pamoja na Naibu Waziri pamoja na watendaji wote kwa kazi wanayoifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali itoe tax period kwa wafanyabiashara wanaotaka kuanzisha biashara zao, ndipo walipe/wakadiriwe mapato. Tatizo watu wanalipa kabla ya kuanzisha biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali iunde Tume Maalum ya kufuatilia viwanda vilivyobinafsishwa na kuona utendaji wake na kuisaidia Serikali kufikia Tanzania ya Viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zinazotolewa na Hazina ni chache na hazifiki kwa wakati, naishauri Serikali itoe fedha kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, utafiti wa masoko kwa mazao yetu nje ya nchi ufanywe kwa umakini na kuwe na mikataba maalumu ndipo uhamasishaji wa kulima zao husika uanze, kuepuka usumbufu kama ulivyotokea katika zao la mbaazi kukosa soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wenye viwanda vinavyotumia sukari ya viwandani wanaidai Serikali bilioni 43.2. Hadi sasa ni shilingi bilioni 13 tu ndizo zilizolipwa, hivyo Serikali iwalipe wafanyabiashara hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ijaze nafasi ambazo watendaji wake wanakaimu ili kuweza kuwa na maamuzi katika masuala mbalimbali ya kiutendaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, viwanda vitumie malighafi zinazopatikana nchini mwetu ili kukuza kilimo chetu, pia kusaidia bidhaa kuwa na bei nafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipunguze utitiri wa kodi kwa watu wanaotaka kuanzisha viwanda ili kuweza kuwapa fursa na wawekezaji wengine kuvutiwa na uwekezaji hapa nchini mwetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, nawaombea afya njema na umri mrefu Mheshimiwa Waziri Joseph G. Kakunda ili kuweza kutekeleza majukumu yao ya kila siku.