Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa hotuba nzuri. Pia nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa utekelezaji wa mkakati wa ujenzi viwanda ili Tanzania ifikie hadhi ya nchi ya uchumi wa kati 2025. Huu ni mkakati wenye tija kubwa sana kwa nchi yetu. Mkakati wa viwanda ni ukombozi kwa vijana wa Tanzania, tatizo kubwa sana la vijana leo ni ajira, viwanda vitaondosha tatizo hili kubwa kwa vijana. Naiomba Serikali iweke msisitizo katika ujenzi wa viwanda vinavyotumia malighafi ya ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imetenga katika Jimbo la Bagamoyo eneo la viwanda kwa awamu mbili, EPZ I (hekta 5,7420 na EPZ II (hekta 3,338). Jumla ni hekta 9,080. Vijiji vitano (5) vimehusika: Zinga, Kondo, Mlingotini, Pande na Kiromo. Maeneo ya EPZ I yamethaminiwa mwaka 2008 ikiwa na jumla ya wafidiwa 2,180. Cha kusikitisha ni kwamba miaka 11 leo wafidiwa 1,025 hawajalipwa fidia yao. Naiomba Serikali yangu Tukufu iwalipe fidia wananchi hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, EPZ II (hekta 3,338) inajumuisha maeneo yenye makazi ya wananchi wengi, zikiwemo Zinga kwa Awadhi, Zinga kwa Mtoro, Kondo, Mlingotini na Kiromo. Vijiji hivi vina jumla ya kaya 3,381 (sensa 2012) zenye watu 12,797. Wananchi hawaridhii kuhamishwa maeneo yao. Naiomba Serikali yangu Tukufu kuwaachia wananchi maeneo yao ya makazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.