Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ubinafsishaji viwanda vya Serikali ambavyo havifanyi kazi hususani viwanda vya Mkoa wa Morogoro mfano Asante Moproco, Canvace, Morogoro Shoes Tanaries na kadhalika, iko haja Serikali kuangalia upya uwekezaji huo kwani kwa sasa kuna malalamiko kuwa wawekezaji wameuza vipuri mfano, Morogoro Canvas vipuri havipo Serikali ifuatilie. Hivi ilikuwa ni uwekezaji, ubinafsishaji au ufilishaji?

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanda cha Tumbaku Morogoro kilichokuwa na uwezo mkubwa wa uzalishaji na kutoa ajira, sasa hivi kimepunguza uzalishaji na ajira na kinadai Serikali tax returns za zaidi ya bilioni 25. Serikali irudishe fedha hizo viwanda viweze kuongeza uzalishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, importation ya bidhaa zinazozalishwa nchini kwa wingi mfano maziwa hatuna sababu ya kuendelea kuruhusu uingizaji wa maziwa ya nje na yanauzwa bei ndogo ikilinganishwa na maziwa yanayozalishwa nchini. Hatuwezi kukuza uchumi kama Serikali haiweki mazingira rafiki kwa viwanda vyetu vya ndani kwa kuvilinda ili viweze kukabiliana na ushindani. Vilevile, returns za tax kwa viwanda vingi hapa nchini hazirudi hii inaweza kushusha fursa za uwekezaji kwa viwanda vingi nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, biashara nyingi zinafungwa kutokana na mazingira magumu ya biashara Kariakoo na katika mikoa mingi. Juzi Mtwara tumeona kwenye TV wafanyabiashara wamerudisha leseni za biashara, hii siyo sawa. Kuna mzigo mkubwa wa kodi mfano OSHA, leseni, tax leavy, Manispaa na kadhalika. Mzigo huu mkubwa wa kodi siyo afya na biashara nyingi zinakufa. Serikali iangalie jinsi ya ku-harmonize hali hii kwani uchumi wa nchi yoyote unategemea mapato yanayotokana na wafanyabiashara wadogo ambao wapo wengi nchini.