Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kutoa mchango wangu katika hotuba hii. Pia nawatakia Waislamu duniani kote Ramadhan Kareem.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga uchumi wa viwanda na ni ukweli usiofichika viwanda vingi vimejengwa. Hata hivyo, kama viwanda havitakuwa na usimamizi mzuri na wataalam wenye ujuzi mkubwa vitakufa na kukosekana kwa matarajio ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima Serikali iweze kuhimiza kujenga viwanda vya kuzalisha malighafi ili kupunguza kupoteza fedha nyingi kuagiza malighafi kutoka nje na kuisababishia Serikali hasara. Mungu ametupa utajiri mkubwa katika nchi hii ikiwemo maziwa na bahari lakini nitazungumzia bahari, tunazo bahari zetu kama Dar es Salaam, Mafia, Tanga, Lindi, Zanzibar lakini bahati mbaya hatuna viwanda vya kuchakata samaki, hii inapelekea kuwakosesha vijana ajira na kupoteza pato kubwa la Taifa. Pia inapelekea leo kuwaachia Wachina kuuza samaki wetu na kuondoka nao. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga viwanda hivi katika Miji niliyoitaja ili tupate maendeleo?

Mheshimiwa Naibu Spika, tunasema Tanzania ni nchi moja na Taifa moja lakini la kushangaza bidhaa zinatoka Zanzibar mfano sukari, maziwa ya Azam, maji ya Drop hayaruhusiwi na hawapewi kibali kuingia Tanzania Bara lakini Zanzibar zinaingia mfano condom, sigara, bia na kadhalika. Nitoe mfano mwingine magari yanayotoka Tanzania Bara ni lazima ulipe ushuru wa bandari TRA na magari yale yale yanapofika Zanzibar yanalipa tena ushuru na TRA. Je, hiyo ni haki? Tunaomba changamoto hii itatuliwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya mchango wangu huo, naomba kuwasilisha.